• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima aikumbusha FEMATA kutunza Mazingira nchini

Posted on: May 5th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amelipongeza Shirikisho la Wachimba Madini nchini FEMATA kwa kupiga hatua na kutoa mchango kwenye Pato la Taifa na kuwakumbusha kutanguliza maslahi ya nchi kwa kuzingatia utunzaji wa Mazingira.


Akizungumza na uongozi na wanachama wa Shirikisho hilo kwenye ufunguzi wa wiki ya Madini inayofanyika kwenye viwanja vya Rock City Mall Jijini Mwanza,Mkuu huyo wa Mkoa amesema anashuhudia mabadiliko ya wachimbaji wadogo hapa nchini kuanzia kwenye vifaa,ajira,kuelimika na mshikamano uliopo miongoni mwao ambao umekuwa na tija kwa maendeleo ya Taifa.


"Bwana Rais wa FEMATA John Bina niseme ukweli kutoka moyoni kwangu hongereni sana kwa hatua mnayopiga,hata mimi nilivyokuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini nikiwa Bungeni nilianzisha kauli ya kuwaita wachimbaji wadogo na siyo wachimbaji wadogo wadogo maana yangu ni watu mnaokwenda hatua kwa hatua hadi kuwa wachimbaji wakubwa"amesema Mhe.Malima


Amewakumbusha FEMATA kuwa wakereketwa wa utunzaji wa Mazingira nchini hasa kutokana na uhalisia wa shughuli zao,kwani wapo baadhi yao hawazingatii hilo na badala yake wanaharibu Mazingira kuanzia kutiririsha maji yenye kemikali ambayo yana hatarisha afya za watanzania,amewahimiza Shirikisho hilo kulipa kipaumbele jambo hilo ili liwe na matokeo chanya.


"Mhe.mgeni rasmi maagizo yako yote tumeyapokea na kukuahidi kuyafanyia kazi,hii wiki ya Madini miongoni mwa mambo tunayofanya ni pamoja na kutoa elimu kwa wanachama wetu ikiwemo utunzaji wa mazingira"John Bina,Rais wa FEMATA.


"Serikali kwa kuendelea kutambua mchango wa Wachimba Madini imeweka mazingira mazuri kwao ya ufanyaji wa shughuli zao ikiwemo kuondoa changamoto zilizokuwa zinarudisha nyuma au kuchelewesha shughuli zao,ndiyo maana sasa wanazidi kupiga hatua na kuwa nguzo ya pato la Taifa" Francis Mihayo,Kamishna wa Madini.


Shirikisho la Wachimba Madini nchini kwa mara ya kwanza linafanya Mkutano wao Mkuu na wiki ya Madini Mkoani Mwanza inayokwenda pamoja na kongamano lenye lengo la kuelimishana na kuzijadili  changamoto mbalimbali zinazowakabili na kushauriana namna ya kuzitatua na pia kutoa

 ushauri na maoni yao Serikalini kuhusu kuyaboresha mazingira yao ya kazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.