• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awahimiza Wana Mwanza kufurika Dimbani Nyamagana Jumamosi hii kuwashangilia wana TP LINDANDA Pamba FC dhidi ya Kitayose

Posted on: March 30th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewahimiza Wananchi wa Mwanza kujenga mshikanano ili timu ya soka ya Pamba FC inayoshiriki ligi ya Championship ishinde mchezo wake wa nyumbani dhidi ya Kitayose siku ya Jumamosi na ipande ligi kuu msimu ujao.

Akizungumza na Vyombo vya habari za michezo ofisini kwake leo kwa lengo la kuwahamasisha wana Mwanza kuelekea mchezo huo dhidi ya Kitayosa,amesema mchezo wa soka hauna miujiza zaidi ya mikakati mojawapo ni wananchi kufurika kwa wingi uwanja wa Nyamagana wanawake kwa wanaume hali ambayo itawaongezea ari wachezaji na hatimaye kutoka na ushindi.

"Niombe nitumie nafasi hii kwa wana Mwanza tujitokeze kwa udi na uvumba katika mchezo huo na hii iwe kwa michezo yote ya nyumbani ukiwemo ule wa Mashujaa FC utakaochezwa Aprili 15 mwaka huu hapo uwanja wa Nyamagana".Amehimiza Mhe.Malima

Amewakumbusha wananchi wa Mwanza wasiwe wazito kuichangia kwa hali na mali timu hiyo kwani kuendesha timu ni gharama na matokeo ya kuipandisha na kucheza ligi kuu yatakuwa na faida kwa wananchi wote wa Mkoa huu ikiwemo burudani ya kuzishuhudia timu mbalimbali na pia kiuchumi.

Tayari Mkuu huyo wa Mkoa ambaye ni mkereketwa wa michezo nchini mwenye sifa ya kuipandisha timu ligi kuu kwenye Mikoa aliyofanya kazi,amesha nunua tiketi 500 na kufanya jumla ya tiketi zilizonunuliwa na wadau wa michezo kufika 1500 ukiwa ni mkakati wa kuwahamasisha wana Mwanza kufurika kwenye dimba la Nyamagana

"Niwakumbushe pia uongozi wa Pamba endapo tutafanikiwa kucheza ligi kuu msimu ujao ni lazima waweke mipango madhubuti kwa kila msimu kuwepo na malengo fulani ili kuhakikisha tunaendelea kubaki tofauti na hapo tutaishia kupanda na kushuka".RC Malima

Katika msimamo wa ligi ya Championship timu ya soka ya Pamba ipo nafasi ya tatu na pointi zake 47 kibindoni huku Kitayose FC kutoka Tabora ikishikilia nafasi ya pili na mtaji wa pointi 49 huku kinara wa ligi hiyo ambao wamejiweka nafasi nzuri ya kupanda ligi kuu msimu ujao  ni wafunga buti wa JKT  Tanzania wakitamba na pointi 56 kileleni.

Pamba FC iliyotamba miaka ya nyuma kuwatoa wachezaji waliokuja kuwa nyota wa timu za Simba na Yanga wakiweno George Masatu,Hussein Marsha , Fumo Felician na marehemu Beya Simba ina miaka 22 haijacheza ligi kuu ya Tanzania Bara.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.