• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awahimiza Wazazi Sengerema kuwapeleka watoto shule

Posted on: January 14th, 2023

*RC Malima Awataka Wazazi Kupeleka watoto Shule Sengerema*


Halmashauri ya wilaya ya Sengerema imekamilisha Ujenzi wa vyumba vya Madarasa 152 yenye thamani ya Tshs Bilioni 3.04 kwa ajili ya wanafunzi wa kidato cha kwanza 2023 ambapo jumla ya wanafunzi 9451 waliofaulu wanaendelea kuripoti na kusajiriwa kwa ajili ya kuanza mwaka wa masomo.

Hayo yamebainishwa leo Jumamosi Januari 14, 2023 wakati wa hafla ya makabidhiano ya Madarasa hayo yakiwa na samani kwenye shule ya Sekondari Nyampulukano ambapo Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amekagua na kupokea Madarasa Matano kwa niaba ya Wilaya nzima.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amewataka wazazi kuhakikisha wanawapeleka watoto wote waliofaulu kidato cha kwanza haraka iwezekanavyo ili wapate elimu bora ambayo Mhe. Rais amewaletea kwa kuwajengea vyumba nadhifu vya Madarasa vyenye Samani.

"Wazazi na walezi hakikisheni watoto wote waliochaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza mwaka huu wanapelekwa shule kufikia Jumanne (Januari 17, 2023), mzazi atayefika jumatano hajapeleka mtoto shule atachukuliwa hatua kali za kisheria maana namna pekee ya kumshukuru Mhe. Rais ni kuhakikisha watoto wanasoma kupitia madarasa haya mazuri aliyotujengea." Mkuu wa Mkoa.

"Mapato ya ndani ya Halmashauri hii hayazidi Bilioni Mbili lakini Mhe. Rais ametuletea zaidi ya Bilioni tatu kwa ajili ya kujenga vyumba vya Madarasa, hii ina maana kwamba tungesema tujenge kwa kutumia mapato ya ndani tusingefanikiwa hivyo namshkuru na kumpongeza sana Mhe. Rais kwa kuupiga mwingi" Mkuu wa Wilaya ya Sengerema Mhe. Senyi Ngaga.

Katibu Tawala Mkoa, Ndugu Balandya Elikana ametoa shukrani kwa Mhe. Rais kwa kuwezesha wanafunzi wote waliofaulu kujiunga kidato cha kwanza kwa wakati mmoja kutokana na fedha alizotoa kujenga vyumba vya Madarasa na miundombinu ya kujifunzia kwa ujumla na ametoa wito kwa watoto kuendelea kuripoti shuleni kutumia fursa hiyo adhimu.

Akitoa taarifa ya Ujenzi, Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo Binuru Shekidele amebainisha kuwa utekelezaji wa mradi huo imefanya Halmashauri kuwa na vyumba 215 wakati mahitaji yalikua vyumba 210 hivyo Halmashauri imekua na ziada ya  vyumba vya Madarasa Matano na ukamilishaji huo utachochea zaidi kuongeza ufaulu kwa wanafunzi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.