• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awakumbusha Viongozi wa Dini kuliombea Taifa Amani,kuliepusha na Maradhi

Posted on: October 6th, 2022

*RC Malima awaomba Viongozi wa Dini kuendelea kuliombea Taifa amani, kuepukana na Maradhi*


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewaomba Viongozi wa Kanisa la KKKT kuendelea kuisadia Serikali katika kuboresha hali za Kiuchumi na za Watanzania kwa ujumla kupitia huduma yao ya Lutheran Mission Corporation (LMC) ambayo lengo lake ni kuratibisha kazi za Umoja za KKKT.

Mhe.Malima ameyasema hayo leo Oktoba 6,2022 alipokuwa akihutubia mkutano wa Majumuisho wa Vyama 13 vya Kimisioni vya kanisa la Kiinjili la Kilutheli kutoka Nchi za Ulaya na Marekani ambapo Tanzania ni sehemu ya waliounda Shirikisho hilo la LMC uliofanyika katika ukumbi wa Hoteli ya Isamilo Jijini Mwanza.

Ameongeza kuwa, KKKT inaweza kushiriki katika kuwawezesha waumini kuunda vikundi mbalimbali vya uzalishaji na kuvisaidia kupata mitaji,kuwa na uongozi bora na kupata elimu ya biashara.

"Wahimizeni kufanya kazi kwa bidii na kwa maarifa wakati wote, wote mnakumbuka kuwa biblia Takatifu kwenye kitabu cha Wathesalonike: 3.10 inatueleza kuwa ikiwa mtu hataki kufanya kazi basi na asile,ni imani yangu kuwa waumini mmoja mmoja au katika vikundi wakiwa na nguvu kiuchumi, kanisa litakuwa na nguvu kiuchumi na vivyo hivyo kwa Serikali," amesema Mhe.Malima.

"Ninaamini kuwa viongozi wa dini mna mchango wenu mkubwa sana katika kuishauri Serikali na kueneza amani katika nchi yetu," ameongeza.

Aidha,Amesiaitiza kuwa, KKKT imeendelea kuwajenga na kuwasadia watanzania kiroho na kimwili kwa kuwawezesha kupata maji safi na salama, elimu na huduma za afya.

Awali akimkaribisha Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Askofu Mkuu wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheli Tanzania Mhe. Dkt. Frederick Shoo amesema anaishukuru Serikali kwa ushirikiano mkubwa kwa kanisa, kwani wamekuwa mchango mkubwa hasa katika madhehebu ya Dini ikiwa ni pamoja na KKKT.

"Mhe Mkuu wa Mkoa kwa kukubali kutenga muda wako katika ratiba iliyonayo kwako wewe kutenga muda wako kwa ajili yetu hakika ni heshima kubwa kwa kanisa letu, "amesema baba Askofu Mkuu Shoo.

Wakati akihitimisha hotuba yake Mhe.Malima amegusia Swala la Mripuko wa Ugonjwa wa Ebola uliotokea Nchi ya Jirani ya Uganda na kusisitiza kuwa mbali na kuchukua tahadhari zote ni lazima Swala la kumshirikisha na  kumuomba Mungu ni la msingi sana pia kuendelea kutoa Elimu maeneo ya ibada ili kuendelea kuchukua Tahadhari.

"Tunaomba muiunge mkono Serikali yenu na muiwezeshe kufanya kazi hiyo, tunaomba ushirikiano wakati wote na tunaomba muendelee kumuombea Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan na kuiombea Serikali kwa ujumla katika sala zenu za kila siku ili iweze kutuongoza kwa haki na kuwaletea Watanzania wote Maendeleo, kwa maana imeandikwa kwenye kitabu cha Mithali: 29.2 kuwa,Wenye haki wakiwa na amri,watu kufurahi, bali mwovu atawalapo,watu huugua, amesisitiza.

Naye Katibu Mkuu KKKT Mhandisi Robert Kitundu akimshukuru Mkuu wa Mkoa huyo amesema kuwa, anamshukuru sana kwa kuwatia moyo kwani kwa Mhe.Malima kufika na  kusema maneno hayo wamejawa na Neema tele na kumuahidi kuwa yeye na wana KKKT wote watabaki wakimuombea.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.