• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awataka TAMESA kusimamia ukarabati wa Vivuko kwa wakati

Posted on: December 19th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima kwa kupitia Kikao cha Bodi ya Barabara amewaagiza Wakala wa Umeme na Ufundi (TEMESA) kuhakikisha wanasimamia ukarabati wa Vivuko na Maegesho kwa wakati ili huduma hiyo muhimu kwa wananchi iweze kurejea kwenye ufanisi.

Akizungumza kwenye kikao hicho leo (Jumatatu Disemba 19, 2022) Mhe. Malima amesema Vivuko Mkoani humo sio anasa wala starehe bali ni huduma muhimu kwa wananchi kutokana na jografia ya uwepo wa makazi mengi kwenye Visiwa hivyo ni lazima kuwe na unyeti katika kuwahudumia.

Ameongeza kuwa vivuko 7 mpaka sasa vipo mikononi mwa Mkandarasi Songoro Marine chini ya usimamizi wa Wakala hiyo hali inayopelekea ugumu kwenye kutoa huduma  kwa wananchi kwenye maeneo mengi kwani ongezeko la abiria ni kubwa tofauti na vyombo vinavyotoa huduma.

Vilevile, amewataka Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kuboresha huduma kwenye uwanja wa Mwanza ikiwemo ukamilishaji wa jengo la kisasa la Abiria na upanuzi wa Barabara ya kutua ndege ili Uchumi ukue kupitia wageni watakaofika Kutalii kwenye hifadhi zinazozunguka kanda ya ziwa kama Serengeti, Burigi-Chato, Saanane, Kigosi na Rubondo.

Akizungumza kwa niaba ya TEMESA, Meneja Vivuko Kanda ya Ziwa na Magharibi Mhandisi Aloyce Ndunguru amefafanua kuwa Taasisi hiyo inaendelea kukarabati vivuko hususani MV Misungwi na maeneo ya maegesho na kwamba taratibu za Manunuzi ya vipuri zinaendelea kwa kushirikiana na Mkandarasi katika kuhakikisha wanakamilisha kazi.

Meneja Mradi kutoka Kampuni ya Songoro Marine William Basiga amesema pamoja na ucheleweshaji wa makabidhiano ya kazi na malipo, kampuni hiyo imejipanga kukamilisha Ukarabati wa vivuko hususani MV Misungwi ambapo tayari wameagiza injini zinazotarajiwa kuingia mwezi januari 2023 ili warejeshe huduma mara moja kwa wananchi.

Aidha, kikao hicho kimewataka pia Mamlaka ya Bandari nchini (TPA) kufuta Ada ya Shilingi 400 wanayotozwa abiria kwa kuingia na kutoka kwenye kivuko cha Buchosa tofauti na ada ya kuvuka wanayotozwa kwani zinawaumiza wananchi kwa kubebeshwa mzigo.

Naye, Meneja wa Wakala wa Barabara (TANROADS) Mkoa Mhandisi Paschal Ambroce amesema hali ya Mtandao wa Barabara kwa asilimia 21.7 ni nzuri hadi na kwamba jumla ya Tshs. Bilioni 16.7 zimetengwa kutengengeneza Kilomita 1,355.88 na Madaraja 5 ndani ya mwaka 2022/23.

"Katika mwaka wa fedha 2021/22 Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA) tulikua na

jumla ya miradi 99 kati ya miradi hiyo 92 imekamilika na Miradi 7 ipo katika hatua za mwisho za utekelezaji kama miradi kiporo ambapo jumla ya Bilioni 27.23 zimetumika" Amesema Meneja wa TARURA Mkoa, Mhandisi Goodluck Mbanga.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.