• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awataka Ukerewe kuongeza kasi ya Miradi ya Maendeleo

Posted on: October 10th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima kwa kushirikiana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa na Wilaya ya Ukerewe amefanya Ziara ya Kikazi kisiwa cha Irugwa na Gana kukagua miradi ya maendeleo.

Akiwa Kisiwani Irugwa  ametembelea shule ya Sekondari  Irugwa ili kujionea miundombinu na hali halisi ya shule hiyo iliyokamilika ujenzi wa vyumba 6 vya madarasa 2021 vyenye thamani ya shilingi milioni 120.

Aidha, Mhe.Malima ameshiriki chakula cha mchana na wanafunzi wa shule hiyo ikiwa ni pamoja na kutoa zawadi ya shilingi laki tatu na thelathini (330,000) na kuahidi kuwapatia wanafunzi wa kidato cha nne Shilingi milioni 1 zitakazowasaidia kipindi cha mitihani, pamoja na Jezi za kiume na kike pamoja na mipira 2 kwa wasichana na 2 kwa wavulana.

Baada ya kukamilisha Ziara yake Kisiwa cha Irugwa Mhe.Malima na Kamati ya ulinzi na usalama alielekea Kisiwa cha Gana Kijiji cha Kamasi,Kata ya Ilangala na kukagua Ujenzi wa Zahanati na kuwapongeza wananchi kwa kuchangia Shughuli milioni 8 kwa ajili ya kununua eneo hilo lenye ukubwa wa mita 50 kwa 60 na kuwataka waendelee kujitoa ili kufanikisha ujenzi huo.

Pamoja na wananchi kuonesha kuunga mkono juhudi za Serikali kuwasaida wananchi wake Mhe.Malima yeye binafsi amechangia ujenzi wa Zahanati hiyo shilingi milioni 1 pamoja na mfuko wa Mkuu wa Mkoa utachangia Shilingi milioni 1 na kuwataka wadau mbalimbali kuendelea kuchangia ili kufanikisha ujenzi huo.

"Serikali uwa inatoa milioni 50 pale ambapo kuna nguvu za wananchi zimeonekana, nendeni mkachangishane kuipa nguvu Serikali ya kuwashika mkono," amesema Mhe.Malima.

Hata hivyo,Mhe Malima ameuagiza uongozi wa Halmashauri ya Wilaya ya Ukerewe kutatua Changamoto mbalimbali zinazokwamisha utekelezaji wa miradi katika Wilaya hiyo ikiwa ni pamoja na maeneo hayo ya visiwani aliyoyatembelea bila kusahau upandaji wa miti ili kutunza mazingira.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.