• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima awataka wawakilishi wa Tanzania michuano ya Kombe la Dunia kwa waishio mazingira magumu kurudi na ubingwa

Posted on: October 3rd, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Adam Malima amewataka wawakilishi wa Tanzania katika michuano ya soka ya Dunia kwa wachezaji wanaotoka katika mazingira magumu itakayofanyika nchini Qatar mwezi huu kuzidi kuonesha uwezo na kurudi na Kombe la ubingwa.

Akizungumza na wachezaji hao kwenye ukumbi mkubwa wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa leo waliofika kumuaga,Mkuu huyo wa Mkoa amesema tangu michuano hiyo ianze mwaka 2010 huko Afrika Kusini, Tanzania imekuwa ikifanya vizuri kwa kushika nafasi za juu hivyo ana imani michuano ya mwaka huu watafanya vizuri.

"Nendeni mkashiriki hii michuano mkitanguliza mambo matatu,kwanza hii ni fursa yenu chezeni kwa uhodari mjulikane,pili wakilisheni vizuri Tanzania, tatu muwe na nidhamu ndani na nje ya michuano hiyo" amesisitiza Mhe Malima.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha wachezaji hao mafanikio yao katika soka hayaji kwa miujiza bali ni bidii na kujitambua nini wanachotaka kufikia malengo.

Kocha mkuu wa timu hiyo Fulgence Novatus amebainisha Tanzania imeendelea kupata heshima ya kualikwa katika michuano hiyo kutokana na kuwa na rekodi nzuri kwani mwaka 2010 huko Afrika ya Kusini walifika hatua ya fainali kabla ya kutolewa na India,mwaka 2014 nchini Brazil walitwaa Ubingwa wa Dunia na mwaka 2018 iliyofanyika Urusi walishika nafasi ya pili kwa upande wa Wanawake.


Nahodha wa timu hiyo Warooba Warooba Kawambule amemuhakikishia Mkuu wa Mkoa Mhe Malima Wana kila sababu ya kurudi na Ubingwa kutokana na uwezo walionao na maandalizi waliyopata.


Timu hiyo yenye jumla ya wachezaji 10 itaondoka kesho kuelekea Dodoma kukabidhiwa bendera ya Taifa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wanawake na Makundi Maalum Mhe Dorothy Gwajima


Michuano hiyo inayochezwa kwenye Viwanja Maalum kwa kila timu kuwa na wachezaji 7 itaanza Septemba 11 hadi 15 mwaka huu ikishirikisha jumla ya Mataifa 28 kutoka Mabarara yote ulimwenguni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.