• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima azitaka Asasi za kiraia kushirikiana na Serikali kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia

Posted on: March 9th, 2023


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amehimiza Asasi za kiraia ziwe mstari wa mbele kwa kushirikiana na Serikali kuelimisha umma kuhusu kutokomeza unyanyasaji wa kijinsia ili jamii iishi kwa upendo na kujenga Uchumi wa nchi.

Akizungumza Wilayani Kwimba katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yalikofanyika ki mkoa Wilayani humo,Mhe.Malima amesema bado kunahitajika jitihada za kutosha za kuelimisha umma hasa kutokana na matendo ya ukatili kwa Wanawake kuzidi kushamiri hali inayotishia kuja na kizazi kijacho kisicho staarabika.

"Wanawake ni nguzo imara sana katika kuchangia Uchumi wa nchi,na wamekuwa mfano mzuri wa kurejesha mikopo wanayopata kwenye Halmashauri,unapo mtenga mwanamke  kiuchumi,kisiasa au shughuli yoyote ya kijamii hatari yake ni kubwa,"amesema Mhe.Malima.

Aidha, Mhe.Malima amewataka wazazi kujenga utamaduni wa kuwa karibu na watoto wao na kuzungumza nao mara kwa mara hali ambayo itawasaidia kujua mapema mienendo michafu inayowakabili.

"Watoto wengi wamekuwa mbali na wazazi wao kwa kuwaogopa, huku wakikabiliwa na vitendo vichafu hii siyo sawa tubadilike, amesisitiza Mhe. Malima.

"Rais wetu Mhe.Dkt. Samia ameonesha mfano wa mwanamke shupavu wa kupigania maendeleo ya Taifa letu, amewapa na anaendelea kutoa nafasi mbalimbali za uongozi kwa Wanawake,wajibu wenu msimuangushe na badala yake mchape kazi kwa bidii kwa kuiga mfano wake," ameongeza Mhe.Ng'wilabuzu Ludigija Mkuu wa Wilaya ya Kwimba.

"Tusisahau kuwekeza kwenye familia zetu, Serikali ya awamu ya Sita imepania kumuinua mtoto wa kike katika mabadiliko ya teknolojia, zitajengwa Shule maalum za kuwapa kipaumbele wanafunzi wa kike ili wasiwe nyuma katika ulimwengu huu wa Sayansi na Teknolojia, kwa hiyo tusijisahau kuziunga mkono juhudi hizi," amesema Mhe.Anjelina Mabula Waziri wa Ardhi,Nyumba na Maendeleo ya Makazi.

"Kila ifikapo Maadhimisho haya tuyatumie kujipima  harakati zetu mbalimbali kwa lengo la kusonga mbele katika nyanja mbalimbali ili tufike katika malengo letu tuliyonuia," amesema Mhe.Merry Masanja Naibu Waziri Mali Asili na Utalii.

Katika Maadhimisho hayo wakina mama wajawazito kutoka kata 30 za Wilaya ya Kwimba wamekabidhiwa majiko ya Gesi kwa lengo la kumuondolea  mwanamke adha ya kutumia muda mrefu kusaka kuni.

Kila ifikapo Macho 8 Dunia huadhimisha siku ya Wanawake huku chimbuko lake likiwa ni kukabiliana na vitendo vya unyanyasaji dhidi yao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.