• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima azitaka Taasisi za Serikali na binafsi kuchangamkia fursa za kiuchumi zilizopo Mwanza

Posted on: September 15th, 2022


Leo Septemba 15, 2022 Katibu Tawala Msaidizi, Mipango na Uratibu Joachim Otaru kwa niaba ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, amezindua Tawi la Kampuni ya Alpha Associates (T) Limited Mkoani humo kwenye hafla iliyoenda Sambamba na Maadhimisho ya Miaka 22 ya Kampuni hiyo.

Akizungumza kwenye hafla hiyo iliyofanyika kwenye ukumbi wa Jengo la Nyanza jijini humo, Ndugu Otaru ametoa wito kwa makampuni binafsi, umma na taasisi mkoani humo kupata msaada kwa huduma na bidhaa mbalimbali zinazotolewa na kampuni hiyo ambayo kwa uwepo wa tawi hilo itakua jirani.

"Nitumie fursa hii kukupongeza sana Dkt. Massaga kwa kuamua kuja kufungua tawi hapa Mwanza na naomba uzoefu mlioutumia kwenye mikoa mingine muutumie kunufaisha makampuni ya hapa Mwanza hasa kwenye nyanja za TEHAMA na ufanyaji wa biashara kwa mfuko rahisi wa kisasa" Amesema, Otaru.

Mkurugenzi wa Kampuni ya Alpha Associates Tanzania Limited Dkt. Alphonce Massaga ametumia siku hiyo adhimu kuwashukuru wafanyakazi kwa ushirikiano, umoja na upendo uliofanikisha ufanisi wa kampuni hiyo kwa kipindi chote cha uhai wa Kampuni.


"Mafanikio yoyote yanaaza kwenye kuthubutu na kuamua kulifanyia kazi wazo lako, kuamini na baadae kuamua kulifanyia kazi wazo lako na kwakweli kwa kupitia maandiko na makongamano mbalimbali yalinijenga na kunifanya leo kufikia hapa kupitia kampuni hii." Amesema Dkt. Massaga wakati akitoa neno la kutokata tamaa.

Mkuu wa Kitengo cha Ushauri kwenye kampuni hiyo, CPA Dalali Njire ametumia wasaa huo kuyakaribisha makampuni kupata huduma kwenye tawi hilo huku akibainisha kuwa kampuni hiyo inatoa huduma za Ushauri wa masuala ya Kodi, huduma za Kihasibu, kukaguliwa masuala ya kifedha na hesabu za mwisho na huduma za sheria.

Awali, Meneja wa Utumishi na Rasilimaliwatu Bi. Anna Zakayo alifafanua kuwa kwa kipindi cha Miaka 22 ya uhai wa Kampuni hiyo wanajivunia kwa kuongoza Ofisi kwa Sera bora kwenye idara mbalimbali za kodi, usalama na utawala kama vile kuajiri na kuhudumia watumishi wao kwa kufuata sheria na miongozo ya nchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.