• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malima kupanda miti milioni 3 Mwanza kukabiliana na upungufu wa uoto wa asili

Posted on: October 7th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amesema yupo katika mkakati kamambe wa kupanda jumla ya miche ya miti milioni 3  Mkoani humo ili kukabiliana na tishio la ukame na kupungua kwa uoto wa asili.

Akizungumza leo na Viongozi na wanachama wa Shirikisho la Walimu Makada wa CCM kwenye Shule ya Sekondari Lugeye Wilayani Magu wakati akiongoza kampeni ya kupanda miche 400 ya miti, Mkuu huyo wa Mkoa amesema   miti ina faida nyingi katika maisha ya Binadamu hivyo kuna umuhimu wa kuitunza.

"Katika maisha ya Binadamu hana mbadala wa chakula na maji ambapo chanzo chake ni uwepo na miti, hivyo vizazi vyetu na vijavyo ni lazima vielimishwe vya kutosha kuhusu umuhimu wa miti," amesema Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Malima amebainisha kuwa Mataifa yaliyoendelea huwezi ukasikia wamekumbwa na ukame hii ni kutokana na kuelimika vyema tangu zamani kuhusiana na thamani ya miti na misitu kwa ujumla.

"Leo naongoza kupanda miche hii 400 lakini nawahakikishia nitakuwa nafuatilia maendeleo yake nikiwa na nia ya kutaka Sekondari hii ya Lugeye iwe ya mfano wa kuigwa kwa kuwa na utitiri wa miti" amesisitiza Mhe. Malima.

Awali akimkaribisha wa Mkoa, Mkuu wa Wilaya ya Magu Mhe, Salum Kalli amesema maagizo yote yaliyotolewa na Mhe Malima kazi yao ni kuyatekeleza hasa wakitambua umuhimu wa miti na mazingira bora kwa mwananchi.

Mwenyekiti wa Shirikisho la Walimu Makada wa Chama cha Mapinduzi Mkoani Mwanza, Jackson Kadutu amesema katika kuiunga mkono Serikali ya awamu ya Sita wameamua kupanda miche hiyo pamoja na kugawa taulo za kike zenye thamani ya Shs milioni mbili na nusu kwa wanafunzi 300 na wengine 150 wenye mahitaji maalum.

"Huu ni utaratibu tuliojijengea kwa muda mrefu na mwaka huu tumefanya hivi pamoja na kukukaribisha rasmi Mkoani Mwanza Mkuu wetu wa Mkoa" amesema Kadutu.

Aidha Shirikisho hilo lenye mchanganyiko wa Walimu wa Vyuo, Sekondari na Msingi, limeshirikisha Halmashauri zote za Mwanza kwa kupanda miche 10,000.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.