• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Malime aagiza aliyeua Albino Kwimba akamatwe haraka

Posted on: November 4th, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima amefika kwenye kijiji cha Ngulla kuwapa pole Bi. Minza Marco (Mjane wa Marehemu), wananchi na wanafamilia kufuatia Kifo cha kikatili cha Ndugu Joseph Mathias (50) kilichotokea usiku wa tarehe 02 Novemba, 2022 baada ya watu wasiojulikana kumkata Mkono wa kulia na kusababisha kifo chake.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Ngulla alipofika kijijini hapo kuwapa pole, Malima amewahakikishia famila hiyo kuwa Serikali itahakikisha watuhumiwa waliofanya tukio hilo wanasakwa na kukamatwa popote walipo na watachukuliwa hatua kali za kisheria.

"Hili jambo ni baya sana na limetutia doa hivyo naliagiza jeshi la Polisi na vyonbo vingine ndani ya wiki moja wanieleze ni kitu gani kilitokea hapa maana wanaoamini kwamba unaweza kutengemeza maisha kwa viungo vya watu wengine naamini walishakwisha ila leo imenidhihirishia kwamba bado mambo haya yapo kwenye jamii." Malima.

Aidha, Malima ametoa Tshs. Milioni Moja kwa familia hiyo kama Ubani na amewataka kuwa na subira na Imani katika kipindi hicho kigumu cha huzuni na kwamba mamlaka zinazohusika zinaendelea na uchunguzi wa mwili na ifikapo ijumaa ya tarehe 04, 11, 2022 watakabidhiwa mwili ili kuweza kumzika.

"Hatuwezi kumrudisha mume wake, ila mkono wa sheria utafuata mkondo wake na hatutawaacha wahuni hao na kuruhusu  wakitembea kwenye ardhi ya Mwanza lazima watakamatwa na kuchukuliwa hatua kali za kisheria," asema Malima.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi wa Ngulla na vijiji vya jirani kutoa ushirikiano kwa jeshi la polisi na vyombo vingine vinavyohusika na uchunguzi kusaidia kutoa ushahidi wa wanachokifahamu kufuatia jambo hilo ili waliotekeleza wanachukuliwe hatua kali za  kisheria na kulikomesha.

"Ndugu zetu hawa wenye ulemavu wa ngozi wana haki ya kuishi ndani ya Mkoa wa Mwanza bila kubughudhiwa na mtu yeyote na hawa Mabwana (Kamati ya Usalama) wakishindwa kuwapata waliofanya tukio hili nitamwomba Mhe. Rais awaondoe wote maana watakua hawatoshi." Amesisitiza Malima.

Kaimu Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa ACP Mairi Makori amesema Marehemu amefariki majira ya saa 5 usiku akiwa amelala na mke wake nyumbani kwake kwenye kijiji cha Ngulla ambapo aliitwa na mtu aliyefika nyumbami hapo na na kugonga mlango huku akimwita jina afungue Mlango na alipotoka nje alishambuliwa na kukatwa mkono wa kulia.


Mwenyekiti wa Chama cha Watu wenye Ulemavu Mkoa, Alfred Kapole ametoa wito kwa wananchi kuacha tabia ya kuua Albino kwani jambo hilo ni baya sana na linatia hofu sana kwa wanachi wenye ulemavu huo na ametoa rai kwa mamlaka husika kuchukua hatua kali za kisheria kwa aliyetekeleza suala hilo.

"Sisi tumeumbwa kwa mfano wa Mungu na wala haijulikani kwamba Mungu alimuumba mtu wa aina gani kwa mara ya kwanza hivyo naomba tumrudie Mungu lakini pia nasi tubaki kuwa salama maana sasa  tutaanza kuomba fedha za kuendesha maisha kwa kuhofia kwenda shambani kulima." Kapole.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.