• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mongella apokea Vifaa tiba kutoka Mradi wa IMPACT kukabiliana janga la corona

Posted on: May 28th, 2020

Aga khan Development Network kwa ufadhili wa serikali ya watu wa Canada (Global Affairs Canada) kupitia mradi wa Improving Access to Reproductive Maternal and Newborn Health (IMPACT)Mwanza wametoa vifaa kinga vya kukabiliana na  maambukizi ya Corona  vyenye thamani ya Million 572,272,498.

Akizungumza baada ya kukabidhi vifaa hivyo kwa Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella, Meneja Mradi wa IMPACT Mwanza Edna Selestine  amesema  fedha hizo zimetolewa na wafadhili kwa ajili ya manunuzi ya vifaa tiba ,vitendea kazi pamoja na kuwezesha mafunzo ya watoa huduma za afya juu ya ugojwa huo pamoja na wahudumu wa afya ngazi ya jamii jinsi ya kuendelea kuelimisha jamii kuendelea kujikinga dhidi ya maambukizi .

Anasema vifaa hivyo vimenunuliwa kwa ushirikianao wa ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza hapahapa Nchini huku msaada huo ukiwalenga watoa huduma za afya na vituo vya kutolea huduma za afya mkoani humo.

Selestine amevitaja vifaa hivyo kuwa ni PPE,150 sets,Barakoa N95 750pcs, Chlorine tablets 100TB -300,surgical masks 35000pcs,Gloves examination,15000pairs na Gloves surgical 3500 pairs,vitakasa mikono 75lts,vitanda vya wagonjwa 30 na magodoro yake pamoja na mabegi 717 ya wahudumu wa afya ngazi ya jamii.

 Aidha Agha Khan inapongeza juhudi zilizofanya na Mhe.Rais Dkt.John Pombe Magufuli  kwa namna alivyokabiliana na vieusi vya corona hadi kufikia hii leo ambapo maambukizi yamepungua kwa kiasi kikubwa.

"Tunatambua kupitia Wizara ya afya kuwa maambukizi ya ugonjwa wa Corona yamepungua nchini pia tumehimizwa kuendeleza jitihada zote za kuendelea kujilinda, mradi wa IMPACT utaendelea kushirikiana na mkoa kila inapowezekana ili kuhakikisha gonjwa hili linatokomezwa kabisa na afya za wananchi zinaendelea kuwa salama" alisema Selestine.

Naye  Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. John Mongella akizungumza baada ya kupokea msaada huo amesema wamekuwa wabia na taasisi hiyo na wameweza kujenga majengo 28 katika vituo vya afya vya sehemu mbalimbali  kwa ajili ya huduma ya mama na mtoto pia vitanda thelathini walivyotoa kwa ajili ya mapambano ya Corona amevigawa 10 Ilemela,Nyamagana 10 na Buchosa 10.

Vilevile aliendelea kuwasihi wananchi kuendelea kufuata maelekezo ya wizara ya afya ,maombi,kutumia miti shamba iliyodhibitishwa sambamba na kupinga nyungu .

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.