• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA KUFUNGWA MFUMO WA KUKUSANYA MAPATO ILI KUDHIBITI UPOTEVU FEDHA BUDUSHI HC

Posted on: September 14th, 2024

RC MTANDA AAGIZA KUFUNGWA MFUMO WA KUKUSANYA MAPATO ILI KUDHIBITI UPOTEVU FEDHA BUDUSHI HC


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemuagiza Katibu Tawala Mkoa kushirikiana na Mganga Mkuu wa Mkoa kuhakikisha ndani ya siku 14 wanaweka mfumo wa makusanyo na matumizi ya fedha kwenye Kituo cha Afya Budushi kilichopo kata ya Sumve wilayani Kwimba.

Ametoa agizo hilo mapema leo Septemba 14, 2024 wakati akifanya ukaguzi wa huduma za afya kwenye kituo hicho na kubaini kuwapo kwa mfumo wa makusanyo na matumzi wa makaratasi badala ya Mfumo wa kisasa wenye ufanisi na unaodhibiti upotevu wa mapato (GOTHoMIS).

Sambamba na hilo, Mhe. Mtanda amemtaka katibu tawala kwa kushirikiana na OR -TAMISEMI kuandaa mafunzo kwa Wakurugenzi wa Halmashauri, Waganga Wakuu wa Wilaya na maafisa TEHAMA ili kuwajengea uwezo wa namna ya kutumia mfumo huo kwa tija na akaahidi kuwa mgeni rasmi kwenye ufunguzi wa mafunzo hayo.

Aidha, ametoa rai kwa Mganga mkuu wa wilaya hiyo kuwa mbunifu na mwenye maamuzi ya haraka katika kufunga mifumo na vifaa tiba na visaidizi kwenye vutuo vya kutolea huduma ili malengo ya serikali ya kuboresha huduma za afya yaonekane mapema.

Akikagua ujenzi hususani kwenye jengo la Mama na Mtoto na kichomea taka ameagiza kasi ya ujenzi iongezwe ili hadi kufikia septemba 30, 2024 wakamilishe na huduma kwa wananchi zaidi ya elfu 17 ziendelee kutolewa katika hali ya ubora na kuwapunguzia msongamano kwenye hospitali ya Kanisa waliyokua wanapata huduma siku za nyuma.

Awali, akiwasilisha taarifa Mganga mfawidhi wa Kituo hicho Paul Kanga amesema mradi wa ujenzi wa kituo hicho umepokea kiasi cha Tshs. 656.4 milioni ambapo Tshs. 300 Milioni kutoka mapato ya ndani ya Halmashauri na Tshs. 356.4 kutoka TASAF ambayo inahusisha na Tshs. 16.5 Milioni za nguvu za wananchi ambao wamenunua pia eneo kwa Tshs. 8 milioni.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.