• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAGIZA VITUO VYOTE VYA AFYA MWANZA KUFUNGWA MFUMO WA GoTHOMIS HARAKA IWEZEKANAVYO

Posted on: January 9th, 2025

RC MTANDA AAGIZA VITUO VYOTE VYA AFYA MWANZA KUFUNGWA MFUMO WA GoTHOMIS HARAKA IWEZEKANAVYO



Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Wataalamu wa afya kusimika na kutumia ipasavyo mfumo wa kielektroniki wa kudhibiti ba kufuatilia taarifa za mteja (GoTHOMIS) ili kuongeza ukusanyanji mapato na utunzaji taarifa za wagonjwa.

Mhe. Mtanda Ametoa agizo hilo mapema leo Januari 09, 2025 wakati akifungua kikao cha mafunzo ya mifumo wa usimamizi wa uendeshaji Sekta ya Afya (GoTHOMIS) ambao unalengo kutunza kumbukumbu na kukusanya mapato kupitia uchangiaji wa huduma kwa jamii.

Amesema katika kutekeleza vema adhma ya mfumo huo ni lazima Wakurugenzi na Maafisa TEHAMA wa Halmashauri kukomesha utoaji wa huduma nje ya mfumo huo mara moja kwa huduma yoyote inayotolewa na kuhakikisha katika kila kituo kinafungwa mfumo huo.

"Mkoa unapimwa kwa usimamizi mzuri wa sera na maagizo ya kisheria, kanuni na afua mbalimbali yanayotolewa na Serikali na siyo vinginevyo, nami sitakubali kuwa wa mwisho kwenye usimamizi wa mfumo huu wa kukusanya mapato na nawataka mkasimamie vizuri." Mkuu wa Mkoa

.

Aidha, amewaagiza kila mmoja kusimamia majukumu yake vema ili kuhakikisha lengo linafikiwa na kwa ambaye atashindwa kufanya hivyo atamchukulia hatua za kinidhamu kwani hatokubali wakati wa tathmini ikionesha mkoa umeshuka.

"Twendeni tukakusanye mapato kupitia mfumo huu maana Serikali imeshasimika miundombinu tena kwa gharama kubwa, mfano katika Mkoa wa Mwanza kwa kipindi kifupi cha uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan tumeshapokea zaidi ya Tshs. Bilioni 49 kwa ajili ya uboreshaji wa miundombinu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Ameongeza kuwa mfumo huo una faida kadhaa ikiwa ni pamoja na mawasiliano baina ya kituo na kituo yaani mgonjwa ataonekana ameshahudumiwa wapi na anahitaji kuongezewa nini bila gharama na pia utunzaji wa taarifa kwa ufanisi.


Halikadhalika, ametoa wito kwa Wataalamu hao kwenda kusimamia suala la mfumo wa iCHF liwe ajenda kwenye vikao na mikutano ya hadhara inayoendeshwa katika ngazi za vitongoji, Vijiji/Mitaa na kata ili wananchi waelimishwe kufahamu faida za kuwa na bima hiyo.

Akitoa taarifa ya awali, Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Dkt. Jesca Lebba amebainisha kuwa Mkoani humo kati ya vituo 354 vinavyopaswa kufungwa mifumo hiyo ni 178 pekee ndio vimefungwa sawa na asilimia 56.2 na hata walikofunga matumizi ni ya kiwango cha chini na akawataka Waganga Wakuu wa Wilaya kuchapa kazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.