• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AAHIDI KUTATUA KERO ZA WAUGUZI MWANZA, AWAHIMIZA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA

Posted on: May 31st, 2024

RC MTANDA AAHIDI KUTATUA KERO ZA WAUGUZI MWANZA, AWAHIMIZA KUTOA HUDUMA BORA KWA WATEJA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameungana na Wauguzi na Wakunga mkoani humo katika Kumbukizi ya mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi Duniani, Florence Nightngale kwa kuwaahidi kutatua baadhi ya kero zao zikiwemo posho za sare za kazi na kupandishwa madaraja

Akizungumza na kada hiyo kwenye Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure Mtanda amesema Serikali inatambua umuhimu na mchango wa wauguzi hivyo Ofisi yake itayafanyia kazi changamoto hizo.

"Mganga Mkuu wa Mkoa na wasaidizi wako nileteeni orodha ya watumishi wanaostahili  kupandishwa vyeo nitakaa na Katibu Tawala kulifanyia kazi na pamoja na hiyo posho ya sare 120,000 kwa mwaka.

Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha kuendelea kufanya kazi kwa weledi wakizingatia viapo vyao huku Serikali ikiendelea kuboresha mazingira yao ya kazi.

"Nimesikia katika risala yenu kuhusu upungufu wa watumishi kwa asilimia 40 hilo lipo kwa Serikali kuu na naamini litaendelea kufanyiwa kazi na Mamlaka husika"Mhe.Mtanda

Naye Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza,Thomas Rutachunzibwa amesema kwenye sekta ya afya bila wauguzi ni sawa na bure na siku zote wanaofanya kazi kwa zaidi ya uwezo wao,hivyo ni vyema wakapewa kipaumbele katika utatuzi wa changamoto zao ili kuwajengea ari ya kazi.

Kwa upande wake Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Bi.Claudia Kaluli amesema licha ya uchache wao ambapo hadi sasa Mkoa una asilimia 60 ya wauguzi,wanaendelea kufanya kazi katika mazingira hayo wakiwa na matumaini ya hali hiyo kupatiwa ufumbuzi na Serikali.

"Ndugu mgeni rasmi siku hii hufanyika kila mwaka na sisi hapa Mwanza kuanzia Mei 29,2024 hadi leo tumefanya shughuli mbalimbali za kijamii ikiwemo upimaji wa Saratani ya shingo ya kizazi,magonjwa yasiyoambukiza pamoja na upimaji wa VVU na kutoa ushauri kwa wateja waliobainika na magonjwa husika na kuwapa ushauri wa kitabibu",Lucia Setembo,M/kiti wa chama cha wauguzi tawi la Seko Toure.

Siku ya Kumbukizi ya mwanzilishi wa taaluma ya uuguzi Duniani,Florence Nightngale imefanyika Kitaifa Mei 12,2024 .mkoani Tanga.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.