• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI YA GESI ILI KAYALINDA MAZINGIRA

Posted on: January 27th, 2025

RC MTANDA AHIMIZA MATUMIZI YA NISHATI YA GESI ILI KAYALINDA MAZINGIRA


Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Mhe. Ng'wilabuzu Ludigija amewakumbusha wananchi kuzingatia matumizi sahihi ya gesi badala ya mkaa ili kuendelea kuyalinda mazingira.

Akizungumza mapema leo asubuhi Januari 27,2025 kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwenye Kijiji cha Mwisonge kata ya Idetetemya wilayani Misungwi wakati wa zoezi la upandaji miti 200 kusheherekea kumbukizi ya kuzaliwa ya Mhe. Dkt.Samia Suluhu Hassan, amebainisha kuwa matumizi ya mkaa ni tishio la ustawi wa mazingira na hewa ya ukaa.

"Leo tunasheherekea kumbukizi ya kuzaliwa ya Rais wetu kwa kumuunga mkono katika suala zima la utunzaji wa mazingira ambapo amesimama kidete kutuhimiza watanzania kutumia nishati ya gesi ili kuepuka ukataji wa miti ovyo," amesisitiza mkuu huyo wa wilaya.

Ameendelea kusema changamoto za tabia nchi na wingi wa hewa ya ukaa unatokana na kutozingatia utunzaji wa mazingira hivyo kuwataka wananchi kuupa kipaumbele kampeni ya mti wa mama kwa kupandi miti kwa wingi.

"Mkoa wetu wa Mwanza mwaka jana tulikuwa na kampeni ya kupanda miti milioni 12 lakini tumeishia milioni 7 sawa na asilimia 60,naamini tutaendelea kushirikiana kuhakikisha Mkoa huu unakuwa wa kijani,"Ludigija.

Kwa upande wake mhifadhi Mkuu kutoka Wakala wa huduma za misitu Kanda ya ziwa TFS,Benard Mwigulu amesema bado wanaendekea kutilia mkazo suala zima la elimu kuhusiana na faida ya upandaji miti kwa kuwashirikisha wanafunzi kama walivyo fanya leo kwenye shule ya Sekondari Mwisonge.

"Leo tumepanda miti ya Maparachichi na Miembe hii ni kumaanisha faida ya miti siyo kimvuli tu bali inawasaidia pia wanafunzi kupata lishe bora kwa kula matunda hali itakayowasaidia kufanya vizuri masomo yao,"Mwigulu.

Balozi wa mazingira nchini Mrisho Mabanzo amebainisha bado mkazo wa kuwahimiza jamii upandaji miti unatakiwa kutokana na zaidi ya asilimia 16 ya ardhi imekuwa ni jangwa.

Mkoa wa Mwanza katika kampeni ya Mti wa mama imepanda jumla ya miti 12000 katika Halmashauri zake 8.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.