• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AIPONGEZA SENGEREMA DC KWA KUPATA HATI SAFI MIAKA 3 MFULULIZO

Posted on: June 17th, 2025

RC MTANDA AIPONGEZA SENGEREMA DC KWA KUPATA HATI SAFI MIAKA 3 MFULULIZO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo tarehe 17 Juni, 2025 ameshiriki kikao maalum cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kujadili hoja za Mkaguzi na Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) katika Halmashauri ya Wilaya ya Sengerema na kuipongeza halmashauri hiyo kwa kupata hati safi ya ukaguzi.

Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Mtanda ameipongeza Halmashauri hiyo kwa kupata hati inayoridhisha kwa miaka mitatu mfululizo na namna ambavyo Halmashauri hiyo imepata hoja chache za ukaguzi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa ameitaka Halmashauri hiyo kutekeleza maagizo na maelekezo ya Kamati ya Bunge ya Fedha za Serikali za Mitaa (LAAC) na hoja nne zilizobakia za ukaguzi sambamba na kulipa fedha zote zilizokopwa.

“Hakuna kuoneana aibu, hakuna kuonea huruma, lazima fedha za mikopo zilizokopeshwa zirudishwe, nataka niwahakikishieni lazima fedha zote zirudishwe dawa ya deni ni kulipa hakuna namna nyingine”. Mhe. Mtanda.

Kadhalika, Mhe. Mtanda ameitaka Halmashauri hiyo kuendelea kujibu hoja za CAG, na kuendelea kushirikiana na Ofisi hiyo kwa kuwa Halmashauri inaye Mkaguzi wa ndani hivyo amewataka kumtumia Mkaguzi huyo ili aisaidie Halmashauri kuweza kujifahamu hali zao kabla Mkaguzi wa nje hajafika.

Mbali na hayo, Mkuu wa Mkoa amesisitiza suala ubunifu amabapo ameitaka Halmashauri hiyo kuweka mikakati ya kubuni na kuanzisha miradi mikubwa ya kimkakati kwa kuwa Halmashauri ya Sengerema ni kubwa na haina mradi wowote wa kimkakati, ameshauri ubunifu huo uongezwe katika Baraza jipya litakaloundwa mara baada ya uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS BALANDYA ATAKA MIRADI YA MAENDELEO KUKAMILIKA KWA WAKATI

    June 17, 2025
  • RC MTANDA AAGIZA HOJA ZA KIMAKOSA KUMALIZWA HARAKA

    June 17, 2025
  • RC MTANDA ATOA MIEZI 2 KWA MANISPAA ILEMELA KUTENGENEZA MAGARI YASIYOTEMBEA

    June 17, 2025
  • RAS BALANDYA ATAKA MIKAKATI KUINUA UFAULU WA WANAFUNZI MAGU

    June 17, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.