• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKABIDHI HATI ZA UMILIKI ARDHI ZILIZOKWAMA KWA TAKRIBANI MIAKA 10

Posted on: July 12th, 2024

RC MTANDA AKABIDHI HATI ZA UMILIKI ARDHI ZILIZOKWAMA KWA TAKRIBANI MIAKA 10


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo julai 12, 2024 amekabidhi hati za umiliki wa ardhi kwa wakazi watatu wa Manispaa ya Ilemela Wilayani Ilemela, waliodai kuhangaikia huduma hiyo kwa muda mrefu, baadhi yao takribani miaka kumi.

Mkuu huyo wa Mkoa aliagiza hati hizo kuandaliwa ndani ya saa 24, baada ya kufanya ziara ya kushtukiza katika Idara ya Ardi ya  Manispaa ya Ilemela Julai 11, 2024, alipokukuta wananchi wengi wakiwa katika foleni ndefu kusubiri huduma na kuamua kuwasikiliza.

Idadi kubwa ya wananchi ilieleza kero ya kuzungushwa na watoa huduma kwa muda mrefu, akamuagiza Kamishna wa Ardhi Msaidizi Mkoa kuandaa hati hizo kwa waliokidhi vigezo haraka iwezekanavyo, ambapo mapema leo amerudi tena wilayani huko kuwakabidhi nyaraka hizo.

Akizungumza mara baada ya kukabidhiwa hati ya umiliki wa ardhi Bi. Immaculata Tenga ambaye pia ni mjane aliyetumia zaidi ya mika tisa kuisaka hati hiyo bila mafanikio, amemshukuru Mkuu huyo wa Mkoa na kusema haikuwa rahisi kwani amekuwa akizungushwa mara kadhaa katika ofisi hizo za ardhi na anaona ni kama ndoto kukabidhiwa hati hiyo siku ya leo.

"Ninakushukuru sana Mkuu wa Mkoa, wewe ni baba katika Mkoa huu, umenisaidia sana nimefanikiwa kuipata hati yangu ambayo nimeisotea kuipata kwa muda mirefu". Bi. Tenga.

Kwa upamde wake Bi. Anna Mbwambo ambaye pia ni majane amesema amesumbuliwa kwa muda murefu na amekuwa akitumia gharama kubwa kwa safari kutoka Dar es Salaam kuja Mkoani Mwanza kufuatilia hati hizo.

"Kwa sasa ninaishi Dar es Salaam nimekuwa na safari za kila wakati kufuatilia hati hii, naona ni kama muujiza nimeipata ndani ya saa 24, Ninakushuru sana Mkuu wa Mkoa". Amesema Bi. Mbwambo.

Akizungumza mara baada ya kuwakabidhi hati hizo Mkuu wa Mkoa amesema wema ni akiba na kuwataka watumishi kuwatendea vyema wananchi kwani thawabu zitapatikana hapa duniani na hata kesho akhera, hakuna haja ya kuwacheleweshea wananchi haki zao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.