• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UONGOZI KUTOKA JIMBO LA HENAN,CHINA

Posted on: September 6th, 2024

RC MTANDA AKUTANA NA KUFANYA MAZUNGUMZO NA UONGOZI KUTOKA JIMBO LA HENAN,CHINA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo amekutana na kufanya mazungumzo na Naibu Gavana kutoka Jimbo la Henan kutoka nchini China,Mhe. Liu Yujiang na kusema mahusiano baina ya Tanzania na China yamezidi kuwa na tija siku hadi siku.

Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika leo Septemba 6,2024 kwenye ukumbi mdogo wa Ofisi ya mkuu wa mkoa ukiwajumuisha Menejiment kutoka pande zote mbili,Mtanda amesema historia ya ushirikiano baina ya Mataifa hayo ni ya muda mrefu na ujio wao utazidi kukuza mahusiano kati ya Mwanza na Jimbo la Henan.

"Ziara yenu ya siku tatu hapa nchini itaongeza tija katika sekta mbalimbali ambazo tumekuwa tukishirikiana yakiwemo masuala ya teknolojia na pia tutabadilishana uzoefu wa kitaalamu kwa maendeleo ya miji yetu",Mkuu wa Mkoa.

Mtanda amebainisha moja ya shabaha kuu ya ziara yao itakuwa ni kutupatia uzoefu wa namna gani mapinduzi na mafanikio ya teknolojia kutoka Jimbo la Henan yatakavyoweza kusaidia Mkoa wa Mwanza katika baadhi ya maeneo kama viwanda na madini na tutakuwa tayari kujifunza kutoka kwao.

Katika mazungumzo hayo yaliyokwenda pamoja na kusaini barua ya kusudio iliyosainiwa na kaimu Katibu Tawala wa mkoa Ndugu Kusirie Swai na mjumbe mmoja aliyeambatana na msafara wa Naibu Gavana huyo,Mtanda ameonesha matumaini ya muendelezo wa ushirikiano huo ambao utazidi kuwanufaisha wananchi kimaendeleo kutoka pande hizo mbili kwa kuibuka fursa mbalimbali za kiuchumi.

Naibu Gavana Mhe.Liu Yujiang amesema licha ya Taifa lao kupiga hatua kubwa kiuchumi Duniani lakini wanajivunia uhusiano na Tanzania na utazidi kudumishwa ili kila upande unufaike katika nyanja zote za kimaendeleo


Waasisi wa muungano wa ushirikiano baina ya Mataifa hayo ni Rais wa awamu ya kwanza wa Tanzania, Hayati Julius Nyerere na Hayati Mao Tsetung kutoka China.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.