• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA MWANZA

Posted on: June 26th, 2024

RC MTANDA AKUTANA NA KUZUNGUMZA NA WAFANYABIASHARA MWANZA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Juni 26, 2024 amekutana na kufanya mazungumzo na baadhi ya Wafanyabiashara wa Mkoani humo lengo likiwa ni kuwasikiliza michango na maoni yao juu ya mgomo wa wafanyabiashara unaoendelea Jijini humo

Katika mazungumzo yake Mkuu huyo wa Mkoa amewataka wafanyabiashara wote waliofunga maduka yao kuhakikisha wanayafungua kwa hiari yao wenyewe kwani Serikali ya Mkoa wa Mwanza ipo tayari kuwasikiliza kama wana hoja za msingi.

"Kama wafanyabiashara mna hoja za msingi njooni tuwasikilize nimekwisha fungua milango kwa makundi yote njooni ofisini mtushauri na mlete hoja zenu na sisi tutaangalia namna sahihi ya kuwasaidia".

"Na kama mkileta hoja zenu zikawa zipo nje ya uwezo wetu sisi tutazipeleka kwa wakubwa wetu huko juu na wao watatupa maelekezo au wao watayatolea maelekezo wao wenyewe," Ameongeza RC Mtanda.

Akizungumza mara baada ya kuwasikiliza Wafanyabiashara hao wanaolalamikia utitiri wa kodi kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza Mhe. Mtanda amesema hakuna Taifa linaloweza kujiendesha bila kodi, Serikali inakuwa na uwezo wa kuwahudumia na kupeleka miradi kwa wanachi kutokana na michango inayotolewa na wananchi wenyewe ikiwemo ulipaji kodi.

"Leo hii Serikali ya Rais samia inafanya miradi mikubwa hapa nchini, je angewezaje kutekeleza hayo kama sio kupitia makusanyo ya kodi kutoka kwa wananchi wake, maendeleo mengi yamefanyika hapa nchini kutokana na  ya makusanyo ya kodi," Amesema RC Mtanda.

Mhe. Mtanda pia amesisitiza kuwa endapo wafanyabiashara hao wanataka sheria za kodi zibadilishwe basi hawana budi kuleta maoni yao ili wabunge wayachukue na wakayafanyie kazi bungeni maana chombo pekee kinachoweza kuunda na kuvunja sheria ni Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.