• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AMEWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI NA KUFANYA KAZI KUJITAFUTIA MAENDELEO

Posted on: June 7th, 2024

RC MTANDA AMEWATAKA WANANCHI KUDUMISHA AMANI NA KUFANYA KAZI KUJITAFUTIA MAENDELEO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi kuimarisha amani na kufanya kazi kwa bidii ili kujitafutia kipato na kuweza kuinua kipato na uchumi wao.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo jioni Juni 07, 2024 kwenye Mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye kijiji cha Misasi katika kata ya Misasi wilayani Misungwi ambapo alibaini uwepo wa vijana wavivu wasioshiriki kazi za kuleta maendeleo na badala yake wanajihusisha na uhalifu.

"Nataka kuona hatua kali zikichukuliwa dhidi ya wananchi wahuni wanaoharibu amani ya watu wengine kwa kujihusisha na wizi, kucheza Pool Table, ujambazi na uvutaji wa bangi na kila aina ya uhalifu" Mtanda.

Akisisitiza kuhusu umuhimu wa kulinda amani, Mhe. Mtanda ametumia wasaa huo kuwaonya Sungusungu ambao hutumika kama askari wa jadi wanaozuia uhalifu kuacha tabia ya kuwakamata na kuwapiga wahalifu badala yake wawafikishe kwenye vyombo ya sheria.

Aidha, ametoa wito kwa wananchi kuacha kuingiza mifugo kwenye shamba la Serikali la mifugo la Mabuki kwani kufanya hivyo kunaharibu juhudi za Serikali za kuinua sekta ya mifugo kwa kuwaletea shamba darasa na ameagiza kutungwa kwa sheria ndogo kali kwa ajili ya kuwaadhibu wanaolisha mazao.

Mwalimu Diana Kuboja, Afisa Elimu wa Sekondari amewapongeza wananchi wa Mwasagera kwa kujenga shule ya sekondari kwa nguvu zao kwa asilimia 100 na imesajiliwa na kwamba ifikapo Julai 01, 2024 watoto wataanza kusoma kwani itafunguliwa.

Dkt. Clement Morabu, Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo amesema kuwa kutokana na uchakavu wa kituo cha Afya wamepeleka ombi maalum la kufanyiwa ukarabati na upanuzi wa kituo hicho na kwamba kwa sasa wamejengewa Jengo la Mionzi kutokana na fedha kiasi walizozipata.

Awali, Diwani wa Kata ya Misasi Mhe. Daniel Busalo amenainisha kuwa ndani ya kata hiyo wameshapokea fedha zaidi ya Bilioni moja kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo na zaidi ya milioni 194 kutokana na fedha za ushuru yaani mapato ya ndani ya halmashauri hiyo.

Awali, Bi. Veronica Heneriko mkazi wa kijiji cha Misasi ameelezea kero ya mmomonyoko wa maadili kwa vijana ambapo amebainisha kuwa wanatumia dawa za kulevya hususani bangi na kwamba wanateseka na adha ya maji na kwamba ni kijiji cha Manawa pekee ndio wanaopata maji.

Martine Mashamba kutoka kijiji cha Mwasagera ameelezea changamoto ya watoto kufuata elimu ya Sekondari kwa umbali mrefu kutokana na kijiji hicho kukosa Shule ya Sekondari na kulazimika watoto kutembea hadi kijiji jirani na kusababisha utoro.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.