• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA SIKU 90 KUKAMILISHA VITUO VYA AFYA MWANZA

Posted on: January 16th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa siku 90 kwa Halmashauri ya Wilaya ya Kwimba kuhakikisha inapeleka fedha za ukamilishaji wa ujenzi wa Vituo vya Afya vya Isunga na Kikubiji akisisitiza kuwa hatavumilia uzembe katika miradi ya maendeleo.

Akizungumza na wananchi wa kijiji cha Isunga baada ya kukagua ujenzi wa majengo ya huduma za afya ulioanza mwaka 2021 Mhe. Mtanda amesema kucheleweshwa kwa ukamilishaji wa miradi hiyo ni dalili ya kutowajibika kwa baadhi ya viongozi wa halmashauri husika.

Amesema Serikali Kuu tayari imetoa shilingi milioni 500 kwa ajili ya Kituo cha Afya Isunga, lakini Halmashauri imetoa shilingi milioni 40 pekee kati ya shilingi milioni 90 zilizotakiwa kuchangia kwa ajili ya ukamilishaji wa ujenzi huo.

“Nitatumia jitihada zangu zote kuhakikisha miradi ya maendeleo katika Mkoa wa Mwanza inakamilika kwa wakati. Mkuu wa Wilaya simamia suala la kuletwa kwa fedha hizi, na ndani ya siku 90 nipate taarifa ya kukamilika kwa mradi huu pamoja na kituo cha Kikubiji.” amesema Mhe. Mtanda.

Ameeleza kuwa kukamilika kwa vituo hivyo kutawawezesha wananchi zaidi ya 4,061 kupata huduma bora za afya ikiwemo huduma za mama na mtoto, upasuaji, maabara pamoja na huduma za wagonjwa wa nje.

Katika hatua nyingine Mhe. Mtanda amewataka wataalamu wa afya kushirikiana na viongozi kuanzia ngazi ya vitongoji kutoa elimu kwa wananchi kuhusu umuhimu wa kujiunga na Bima ya Afya kwa Wote, ili kuongeza upatikanaji wa huduma za afya kwa gharama nafuu.

Amesisitiza kuwa elimu hiyo ni sehemu ya utekelezaji wa malengo ya siku 100 za Serikali ya Awamu ya Sita yenye lengo la kuboresha huduma za kijamii na kuongeza ustawi wa wananchi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA: DHAMIRA NI MSINGI WA KUFANIKISHA SHUGHULI ZA MWENGE WA UHURU 2026

    January 26, 2026
  • NDC WAHITIMISHA ZIARA YA MAFUNZO MWANZA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AZINDUA MELI MPYA YA MV NEW MWANZA, ATOA MAAGIZO KWA MIRADI ILIYOSIMAMA

    January 23, 2026
  • WAZIRI MKUU AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA MAJI SAHWA -MWANZA

    January 23, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.