• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA ATOA WITO KWA COPRA KULETA MAGEUZI CHANYA MAZAO MCHANGANYIKO

Posted on: January 8th, 2025

RC MTANDA ATOA WITO KWA COPRA KULETA MAGEUZI CHANYA MAZAO MCHANGANYIKO


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda leo Januari 8, 2025 amefanya mazungumzo ofisini kwake na uongozi kutoka Mamlaka ya udhibiti wa nafaka na mazao mchanganyiko (COPRA) na amewataka kuleta mageuzi chanya kwenye mazao inayosimamia.

Ujumbe huo ukiongozwa na Mkurugenzi wa Taasisi hiyo mpya iliyopo chini ya Wizara ya Kilimo, bi. Irine Mlola katika mazungumzo na mwenyeji wao umeombwa kuhakikisha inawaleta wataalamu bora ambao wataongeza tija ya mazao yaliyokusudiwa ambayo ni nafaka na jamii ya mikunde.

"Hongereni kwa kuja na mpango huu mzuri maana tangu miaka ya nyuma tulikuwa tunasikia mazao ya biashara na chakula, lakini ukweli ni kwamba sasa kilimo chote ni biashara hayo mazao yaliyokosa usimamizi naamini yataingia kwenye mnyororo wa thamani," RC Mtanda.

Aidha, Mkuu huyo wa Mkoa ameihakikishia Taasisi hiyo kwa kushirikiana na Ofisi yake kuwakusanya wadau wa mazao ya nafaka na mikunde ili kuwajengea uelewa wa taasisi hiyo na makusudi yake kwenye kilimo hicho kwa ujumla.

"Mhe. Mkuu wa Mkoa lengo la ujio wetu kwanza ni kujitambulisha na kukufahamisha majukumu ya taasisi hii ambayo ilianzishwa mwaka 2023 na kuanza rasmi kazi mwaka jana, kusimamia shughuli za masoko kwa mfumo wa stakabadhi gharani kwa mazao 5-6 yakiwemo Kokoa, Ufuta, Soya, Mbaazi, Dengu na mwaka huu 2025 tumeongeza zao la Choroko", Irine Mlola, Mkurugenzi COPRA.

Uongozi huo umepita mikoa ya kanda ya ziwa na jirani kwa lengo la kuitambulisha Taasisi hiyo na kufungua Ofisi zao.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MWANZA, SIMIYU ZANG'ARA UTAMILIFU DARASA LA SABA KANDA YA ZIWA

    May 30, 2025
  • RAS MWANZA AZINDUA RASMI MRADI WA KUPAMBANA NA UGONJWA WA SELI MUNDU

    May 30, 2025
  • WAANDISHI WA HABARI MWANZA WAPIGWA MSASA MIKAKATI YA KUTOKOMEZA WATOTO WA MITAANI

    May 29, 2025
  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.