• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAAGIZA JIJI LA MWANZA KUMPA KAZI MKANDARASI ATAKAYEWEZA KUJENGA SOKO LA MCHAFU KUOGA USIKU NA MCHANA

Posted on: June 3rd, 2024

RC MTANDA AWAAGIZA JIJI LA MWANZA KUMPA KAZI MKANDARASI ATAKAYEWEZA KUJENGA SOKO LA MCHAFU KUOGA USIKU NA MCHANA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka Halmashauri ya jiji la Mwanza kuhakikisha wanampata Mkandarasi atakayefanya kazi usiku na mchana katika mradi wa ujenzi wa soko la wafanyabiashara wadogo la mchafukuoga ili lijengwe kwa kasi.

Amesema hayo leo Juni 03, 2024 wakati akiwa kwenye ziara ya ukaguzi wa huduma kwenye soko hilo lililopo kata ya Igogo na akabainisha kuwa ndani ya miezi sita wananchi watapata soko la kisasa lenye miundombinu ya Maji, Vyoo na nishati ya Umeme.

Amesema, ni lazima Halmashauri ihakikishe inalinda fedha zinazotolewa na Mhe. Rais kwa ajili ya ujenzi wa miradi na kwamba yeye kama msimamizi hatokubali kuona fedha za umma zikichezewa na watu wachache kwa kufanya ubadhirifu na atakayethubutu atamchulia hatua za kisheria.

Aidha, amebainisha kuwa Serikali itasaidi kuweka utaratibu wa kuwaunganisha wafanyabiashara wa Kanda ya ziwa ili kulifanya Soko hilo kuwa kitovu cha Uuzaji wa Mitumba ya nguo na kwamba hali hiyo itasaidia hata kuleta watalii kwenye soko hilo.

Hatahivyo, amezitaka Mamlaka zinazohusika na maji yaani MWAUWASA, TANESCO-Umeme, TARURA kwa ajili ya barabara pamoja na Halmashauri kuboresha huduma zote zinazowahusu  ili wafanyabiashara hao wapate ridhiki kwenye eneo linalofaa na wasihatarishe afya zao.

Awali, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mhe. Amina Nyamagana alibainisha historia ya uwepo wa wafanyabishara hao kuwa ni kutokana na kupangwa kutoka uuzaji holela waliokua wakishiriki siku za nyuma kwa kuuza nguo mjini kwenye hifadhi ya barabara.

Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Jiji la Mwanza Peter Lehhete amemhakikishia Mkuu wa Mkoa kuwa siku za karibuni atapatikana Mkandarasi wa ujenzi wa Soko hilo kwani tayari Halmashauri ipo kwenye taratibu za manunuzi na kwamba wametenga shilingi Bilioni 7 kujenga soko la Kisasa.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.