• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWAALIKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO KUTOKA TADB

Posted on: December 3rd, 2025

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka vijana na makundi mengine mkoani humo kuchangamkia fursa za kujiajiri katika kilimo, uvuvi na ufugaji ili waweze kupata mikopo isiyokua na riba kupitia benki ya maendeleo ya kilimo (TADB) inayosimamiwa na serikali.

Amebainisha hayo leo Disemba 3, 2025 wakati akifungua mafunzo yaliyoandaliwa na Benki ya maendeleo ya kilimo Tanzania (TADB) kwa Waandishi wa Habari mkoani humo ambapo ametumia wasaa huo kuwaalika wananchi kwenda kukopa na kufanya shughuli za uzalishaji.

Mhe. Mtanda amesema kwa kipindi cha mwaka 2024/25 jumla ya Tshs. Bilioni 7.5 zimekopeshwa bila riba na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kwa vijana 350 wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi wa kisasa wa kutumia vizimba walio katika vikundi 47 ambapo tayari Bilioni 1.3 wamerejesha kwa awamu ya kwanza.

“Jumla ya Tshs. Bilioni 7.5 zimekopeshwa bila riba na Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) kwa vijana 350 walio katika vikundi 47 mkoani Mwanza katika kipindi cha 2024/25 wanaojishughulisha na shughuli za uvuvi wa kisasa wa kutumia vizimba”. Amesema Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka wanahabari pia kuchangamkia fursa na kuunda vikundi vyao ili waweze kupata fursa ya kukopeshwa na kurejesha bila riba na waweze kujikwamua kiuchumi kwakua kwa miaka 10 tangu kuanzishwa kwa benki hiyo imekua hodari wa kuwawezesha wajasiriamali.

Akizungumza na wahariri na waandishi wa habari meneja wa TADB kanda ya ziwa Bw. Alphonce Mokoki amesema benki yao inalengo la kuwawezesha wakulima ili waweze kutoka katika kilimo cha kujikimu na kwenda katika akilimo cha biashara pamoja na kuiwezesha nchi kuwa na chakula cha kutosha.

Ameongeza kuwa benki hiyo imekua kinara wa kuwafungulia fursa vijana na kwamba zaidi ya Tshs. Bilioni 79.14 zimekopeshwa kwa makundi ya wafugaji, wakulima na wavuvi mkoani humo na wote katika mnyororo huo wa thamani.


Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RC MTANDA AWAALIKA VIJANA KUCHANGAMKIA FURSA ZA MIKOPO KUTOKA TADB

    December 03, 2025
  • RC MWANZA AKUTANA NA VIONGOZI & WACHUNGAJI WA AICT ASISITIZA AMANI NA MSHIKAMANO

    December 02, 2025
  • TUWE WABUNIFU KWENYE KAZI TUSISUBIRI KUELEKEZWA- RAS BALANDYA

    December 02, 2025
  • RC MTANDA AZITAKA KAMATI ZA USHAURI WA KISHERIA KATIKA MKOA WA MWANZA KUMALIZA NA KUTATUA MIGOGORO YA WANANCHI

    December 02, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.