• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA BODABODA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA

Posted on: November 9th, 2024

RC MTANDA AWATAKA BODABODA KUSHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka maafisa usafirishaji wa pikipiki za abiria (Bodaboda) Mkoani humo kufuata sheria za usalama wa barabarani ili kujiepusha wao na abiria wanaowabeba na ajali za barabarani.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo leo  Novemba 09 2024 katika ukumbi wa Nyanza jijini Mwanza wakati akifungua Mkutano mkuu wa jumuiya hiyo ambapo wanakwenda kuchagua viongozi katika ngazi za kanda, mkoa na wilaya wa kundi hilo.

"Nawasihi sana twendeni tushirikiane kuzuia ajali, tutambue kwanza kuwa hatuvai kofia ngumu (helmet)kwa ajili ya kumfurahisha askari wa barabarani (trafiki) bali ni kwa faida yetu wenyewe." Mhe. Mtanda.

Aidha, amewataka kuwa walinzi wa amani baina yao kwa kuhakikisha kila mmoja anamfahamu mwenzake na anapoona mwenendo mbaya unaoashiria uhalifu basi mara moja atoe taarifa katika uongozi wa serikali ya mtaa.

Ametumia wasaa huo kuwataka pia kuacha tabia za kuchagua viongozi ambao ni wababe na wabishi kwa ajili ya kuwaandaa kubishana na viongozi wa wilaya bali wakachague viongozi waadilifu  ili wawasaidie siku za usoni.

"Twendenu tukashiriki uchaguzi wa serikali za mitaa siku ya jumatano  Novemba 27, 2024 na pia tunaimarishe usalama katika kipindi chote cha uchaguzi huu." Amesisitiza Mkuu wa Mkoa.

Mhe. Mtanda ameichangia jumuiya hiyo inayoendesha shughuli zao na kaulimbiu isemayo 'Bodaboda Usafiri Salama' Tshs. 500,000 kwa ajili ya kuwaongezea nguvu katika majukumu yao

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.