• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA WANAOFANYA MNADA BARABARANI KURUDI KWENYE SOKO RASMI LA KILOLELI

Posted on: June 5th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WAFANYABIASHARA WANAOFANYA MNADA BARABARANI KURUDI KWENYE SOKO RASMI LA KILOLELI


Mhe. Said Mtanda, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza amewataka wafanyabiashara wilayani Ilemela kufuata sheria za nchi kwa kufanya shughuli zao kwenye masoko rasmi na Halmashauri isimamie hilo kwa kupunguza Minada ya barabarani na kuhamasisha wabaki kwenye masoko yaliyopangwa.

Ametoa agizo hilo leo tarehe 05 juni, 2024 wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Soko la Kiloleli lililopo kwenye kata ya Ibungilo wilayani Ilemela baada ya kubaini wafanyabiashara wadogo kususia Soko hilo lenye miundombinu rafiki na kujikita kwenye magulio ya mnada yanayofanyika kwenye hifadhi za barabara.

"Kukaa kwenye masoko kuna faida kubwa ya kwanza ikiwa ni kutambulika nani yupo wapi na anafanya biashara gani, watu wafuate sheria wakae kwenye masoko sio kuendekeza minada inayofanyika barabarani, tupunguze magulio ili mabenki wajue wanawapata wapi kuwakopesha na hata Mikopo ya Rais Samia ikishakua tayari itakua rahisi kuwapata." Amesisitiza Mhe. Mtanda.

Akibainisha Miradi mikubwa inayotekelezwa Mwanza, Mtanda amesema Soko Kuu la Mjini Kati linalojengwa kwa zaidi ya shilingi Bilioni 20 linaelekea kukamilika na kwa sasa limefikia 95% ya ujenzi na Serikali inatarajia kuongeza Bilioni 3 ndani ya mwezi huu ili likamilike na waganyabiashara zaidi ya elfu mbili watarudi kuendelea na biashara kwenye soko lile la kisasa.

"Nimetoa wito kwa maeneo yote niliyopita kwamba Askari wa Jeshi la akiba kazi yao sio kupiga wananchi na kunyang'anya biashara nasi tutawafikisha mahakamani wanaofanya hivyo bali wanapaswa kukamata na kuwafikisha kwenye vyombo husika." Mkuu wa Mkoa.

Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Mhe. Hassan Masala amesema wapo tayari kutekeleza maagizo hayo na kwamba wamejipanga kuboresha miundombinu kwenye masoko yao na kwa mwaka wa fedha unaoendelea wametumia zaidi ya Milioni 180 kukarabati miundombinu kwenye masoko lakini bado machinga wamejikita kufanya biashara kwenye hifadhi za barabara kwa kigezo cha mnada.

Magabe Ligata, mwenyekiti wa Soko la Kiloleli na mwenyekiti wa Wafanyabiashara na Masoko wilayani Ilemela ametoa kwa wafanyabiashara wenzake kurudi kwenye soko hilo ili maeneo ya nafaka, ndizi, matunda na nguo yapate wafanyabiashata kuliko hali ya sasa ya kuwa na wafanyabiashata 386 pekee kwenye soko hilo.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.