• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUSIMAMIA UPATIKANAJI WA DAWA KWA KARIBU

Posted on: June 26th, 2024

RC MTANDA AWATAKA WAGANGA WAKUU WA MIKOA NA WILAYA KUSIMAMIA UPATIKANAJI WA DAWA KWA KARIBU


kutokana na kuwepo kwa malalamiko mengi juu ya wizi wa dawa, kununua dawa nyingi na hatimaye kuchina na kusababisha hasara kwa Serikali, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka na kuwaagiza Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya za Kanda ya Mwanza kuhakikisha wanasimamia upatikanaji wa dawa kwa karibu.

Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo wakati akihutubia katika mkutano wa mwaka na wadau wa afya kanda ya Mwanza uliofanyika leo Juni 26, 2024 mkoani humo,Mhe. Mtanda amewataka waganga wakuu wa wilaya na Wafamasia wa mikoa kukagua na kufuatilia matumizi ya bidhaa za afya katika kila ngazi ili kudhibiti mianya ya upotevu wa bidhaa hizo.

"Ni mategemeo yangu kuwa baada ya mkutano huu, wote tutaondoka na uelewa wa pamoja na maazimio ambayo utekelezaji wake utaboresha upatikanaji wa bidhaa za afya pamoja na kuboresha huduma za afya maeneo yetu ya kazi".

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa amewakumbusha wadau wa MSD kupitia Wizara ya afya, kufanya maoteo ya bidhaa za afya kwa usahihi, weledi na kwa wakati, hii itawezesha MSD kuwa na takwimu sahihi katika bidhaa za afya kuagiza kutoka kwa wazalishaji na washitiri hivyo kuboresha upatikanaji wa bidhaa hizo.

Kadhalika Mhe. Mtanda amewataka waganga wakuu wa wilaya na wafamasia kusimamia ukusanyaji wa mapato katika vituo vya kutolea afya ili vituo hivyo viweze kulipa madeni yaliyopo MSD kwa wakati mara baada ya kupokea shehena ya bidhaa na kuepusha madeni yasiyo ya lazima.

"Ninawakumbusha pia mna jukumu la kuvisimamia vituo vya kutolea huduma za afya katika maeneo yenu ili viweze kukusanya mapato ya kutosha yanayotokana na uchangiaji wa huduma za afya".Mkuu wa Mkoa

Naye Mwakilishi wa Mkurugenzi Mkuu wa Bohari ya dawa (MSD) Bw. Victor Sungusia amesema mikutano ya mwaka na wadau wa afya ni muhimu sana kwa pande zote mbili yaani MSD yenyewe na viongozi wa sekta ya afya ngazi ya Mkoa na Wilaya, kwa sababu wakati wa kikao hicho kuna mambo yatawasilishwa na kujadiliwa ambayo ni muhimu wakati wa utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.