• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Prime Minister's Office Regional Administration and Local Government Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AWEKA MSISITIZO MKALI UJENZI WA GOROFA TANO HOSPITALI NYAMAGANA UONGEZEWE KASI

Posted on: February 12th, 2026

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemtaka mkandarasi HUMPHREY CONSTRUCTION LIMITED kuongeza kasi ya ujenzi wa jengo la ghorofa tano katika Hospitali ya Wilaya ya Nyamagana kwa kufanya kazi usiku na mchana ili mradi huo uanze kutoa huduma haraka.

RC Mtanda amesema Serikali imetoa zaidi ya shilingi bilioni 2 kwa mradi huo, huku mkandarasi akiwa tayari amechukua zaidi ya milioni 900, lakini kasi ya utekelezaji hairidhishi na idadi ya wafanyakazi ni ndogo.

Kwa mujibu wa mkataba, mradi ulipaswa kukamilika Januari mwaka huu, lakini hadi sasa umefikia takribani asilimia 83 ya utekelezaji. RC amemtaka mkandarasi kuhakikisha ifikapo tarehe 11 Machi anakamilisha awamu ya kwanza kama ilivyokubaliwa.

Ameonya kuwa kushindwa kutekeleza mradi kwa wakati kutasababisha mkandarasi huyo kukosa awamu ya pili na hatua za kisheria zitachukuliwa.

Vilevile, amemtaka Mkandarasi Mshauri, ATC Production and Consulting Bureau PLC ya Arusha, kutoa taarifa za mara kwa mara za maendeleo ya mradi na kusimamia ubora ili kuepuka kasoro za ujenzi.

Akitoa taarifa ya mradi, Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Nyamagana, Dkt. Halima Basila amesema jengo hilo litatoa huduma za dharura, ICU, maabara, mionzi, upasuaji, kliniki za macho na meno, wodi za wazazi, wodi binafsi pamoja na ofisi za utawala.

Mradi huo wa siku 365 ulianza Novemba 2024. Hadi sasa zaidi ya shilingi milioni 826 zimetumika kwa mkandarasi mshauri na mjenzi, huku gharama ya mradi mzima ikikadiriwa kufikia zaidi ya shilingi bilioni 14. Serikali Kuu imeshatoa zaidi ya shilingi bilioni 2 kwa awamu mbili kusaidia utekelezaji wake.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • MKURUGENZI IDARA YA MAAFA OWM AFUNGA MAFUNZO YA KUKABILIANA NA DHARULA MWANZA

    February 20, 2026
  • KAYA 19,344 KUNUFAIKA NA BIMA YA AFYA KWA WOTE MWANZA AWAMU YA KWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AMPOKEA WAZIRI DEUS SANGU MWANZA

    February 20, 2026
  • RC MTANDA AWATAKA WASIMBE NA WABANZA KUUNGANA KUKATA BIMA YA AFYA KWA WOTE

    February 20, 2026
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.