• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA AZITAKA NCHI WANACHAMA KUENDELEA KUDHIBITI UHALIFU UKANDA WA ZIWA VICTORIA

Posted on: May 21st, 2024

RC MTANDA AZITAKA NCHI WANACHAMA KUENDELEA KUDHIBITI UHALIFU UKANDA WA ZIWA VICTORIA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ametoa wito kwa nchi wanachama kuendelea na uthibiti na jitihada za kuondoa vitisho na uhalifu kuzunguka ziwa Victoria ili kuwaletea wananchi maendeleo kupitia shughuli za kiuchumi za uvuvi wanazofanya.

Mhe. Mtanda ametoa wito huo mapema leo Jumanne 21 Mei, 2024 wakati akifungua kikao kazi cha tatu cha kuimarisha usalama wa raia wanaofanya kazi katika ziwa Victoria kutoka Kenya, Uganda na Tanzania kilichoandaliwa na Shirika la Kimataifa linalihusika na masuala ya Uhamiaji (IOM).

"Wananchi wa Kenya, Uganda na Tanzania wanajivunia na uwepo wa ziwa Victoria lenye maji safi duniani na ni kitovu cha biashara na maisha kwa ujumla hivyo ni lazima tuhakikishe tunaandaa mipango ya kuhakikisha tunaondoa vitisho vyote vya kiusalama chini ya wadau wetu Serikali ya Marekani kwa kupitia mradi wa IOM", Mhe. Mtanda.

Amesema, ni wajibu wa Serikali za nchi zote tatu kuwa na mipango ya muda mfupi na mirefu ya kuhakikisha matukio mbalimbali yanayotishia amani kwa kuwa na uhalifu mipakani yanazuiliwa na kwamba kamisheni mbalimbali zinazofanya kazi kwenye bonde la ziwa hilo zinatakiwa kuwa msaada pia kwenye suala hilo nyeti.

Aidha, ametoa wito kwa wizara zinazohika na masuala ya usalama na undelezaji maliasili maji kutoka kwenye nchi wanachama kuweka mipango ya muda mrefu kupitia bajeti za nchi wanachama kuhakikisha utapoisha mradi wa IOM kunakua na muendelezo wa juhudi za uthibiti wa uhalifu kwenye mipaka ya ziwa Victoria.

Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa, Mwenyekiti anayemaliza muda wake Kamishna Msaidizi wa Uhamiaji kutoka Uganda Marcellino Kyamutetera amesema kwa kipindi chote akiwa kwenye uongozi amehakikisha nchi wanachama zinaongeza mahusiano ya kikanda katika kuhakikisha wanazuia kwa pamoja uhalifu wa mipakani.

Ndugu David Hofmeijer kutoka IOM Ofisi ya Tanzania amesema kikao kazi hicho kinalenga kuimarisha uhusiano na kukumbushana namna bora ya kuendelea kuboresha ulinzi kwenye mipaka ya nchi wanachana yanayolenga kukabiliana na uhalifu wa Kimataifa na tishio kwenye mipaka ya nchi wanachama.

Akitoa neno la ukaribisho, Kamishna Msaidizi kutoka Sekretarieti ya kupambana na usafirishaji wa binadamu (ATS) Ahmad Mwen-dadi ametumia wasaa huo kuwashukuru IOM na nchi wanachama kwa kuendelea kulinda mipaka ya nchi na kufanikisha malengo ya mradi huo.

Ameendelea kwa kusema bandari za nchi wanachama zote zipo salama ikiwa ni kutokana na ushirikiano mkubwa uliofanywa kwa pamoja kutoka 2023 ambao IOM imekua ikitoa mafunzo ya kuwajengea uwezo maafisa kutoka majeshi ya Uhamiaji, Polisi na wanamaji na kwamba mradi huo una msaada sana kwenye kuimarisha biashara na forodha.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.