• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MTANDA: MALEZI YA MABAVU CHANZO CHA KUMJENGEA HOFU MTOTO

Posted on: June 16th, 2024

RC MTANDA: MALEZI YA MABAVU CHANZO CHA KUMJENGEA HOFU MTOTO


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Bw.Balandya Elikana  amewataka Wazazi na Walezi kuzingatia wajibu wa malezi bora kwa watoto maana  yana mchango mkubwa  katika kuwajengea maadili mema.

Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza leo Juni 16,2024 kwenye ukumbi wa Gold Crest katika siku ya maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika,Balandya amebainisha malezi sahihi ni kujenga urafiki na ukaribu na mtoto na siyo vinginevyo.

Mtendaji huyo wa Mkoa amesema Wazazi wengi wanaamini kuwa matumizi ya nguvu na ukali (malezi ya mabavu) ndio njia sahihi ya malezi kwa watoto ambapo amesema madhara ya njia hiyo ni kumjengea hofu mtoto hivyo kuondoa dhana ya uthubutu katika ubunifu.

"Pia matumizi ya nguvu yanaweza kuudhuru mwili wa mtoto, vile vile mtoto anaweza kuathirika kisaikolojia madhara ambayo yanaweza kudumu maisha yake yote".amesisitiza Balandya

Aidha  ametoa rai kwa wazazi kuachana na malezi ya kuwadekeza watoto kwa kuwapatia chochote wanachohitaji hata kama sio muhimu ambapo amesema madhara yake ni kumjengea mtoto mtazamo kuwa kila kitu kinapatikana kirahisi.

"Hisia hizo zinaweza kuendelea katika maisha yake yote, kujenga familia na taifa la kuamini katika njia za mkato na sio kupata kwa jasho - Tunashuhudia wizi na ubadhilifu ili kutimiza azma hiyo".

Akisoma risala ya watoto wa Mkoa wa Mwanza kwa mgeni rasmi, mtoto Josephine Bakita amesema wanaipongeza Serikali katika kuhakikisha watoto wanapata haki za msingi hususani elimu kwani imefanikiwa kujenga shule nyingi nchini na kuweka mfumo wa elimu bila malipo kwa Shule zote, watoto wengi wenye mahitaji maalumu na wasio na mahitaji maalumu wanapata elimu sawa.

Sambamba na hayo pia amewasilisha changamoto zinazowakabili watoto amesema wamekuwa wakikabiliwa na uhaba wa miundombinu rafiki kwa watoto wenye mahitaji maalumu shuleni, upungufu wa vifaa vya kujifunzia na kufundishia pamoja na uhaba wa Walimu wenye taaluma ya elimu jumuishi.

Akijibu baadhi ya changamoto zilizowasilishwa  Balandya amesema kuwa Serikali Mkoani Mwanza kwa kushirikiana na sekta binafsi wamekuwa wakishirikiana katika upatikanaji wa vifaa mbalimbali vya kujifunzia hivyo kama kuna mtoto yoyote mwenye uhitaji basi afike Ofisi ya Mkuu wa Mkoa aweze kupatiwa vifaa hivyo, aidha suala la uhaba wa walimu na miundombinu rafiki amesema ameyachukua kwa ajili ya utekelezaji.

Kauli mbiu ya Maadhimisho ya siku ya Mtoto wa Afrika kwa mwaka 2024 ni "Elimu Jumuishi kwa Watoto Izingatie Maarifa, Maadili na Stadi za Kazi.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.