• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza aomba CAG kuja kukagua mchakato wa fedha za Mikopo kwa Makundi Maalum Halmashauri ya Jiji la Mwanza.

Posted on: May 30th, 2022

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa agizo kwa Katibu Tawala wa Mkoa huo Ngusa Samike kumuandikia barua Mkaguzi na Mdhibiti wa Hesabu za Serikali CAG kuja Mwanza na kuchunguza mwenendo mzima wa Vikundi vyote vilivyopatiwa Mikopo ya Makundi Maalum na Halmashauri ya Jiji la Mwanza baada ya kubainika zaidi ya Shilingi Bilioni 3 kutolewa nje ya utaratibu.


Mhe Gabriel ametoa agizo hilo baada ya kupata taarifa ya mwenendo wa utoaji wa Mikopo hiyo kutoka Kamati Maalum aliyoiunda ili kuchunguza mchakato wa utolewaji wa  fedha hizo iliyobaini Vikundi 156 ndiyo Halmashauri hiyo ina taarifa zao kati ya 337 kutoka kata 10 miongoni mwa 18 zilizopo ndani ya Wilaya hiyo.



"Nimelazimika kuitisha kikao hiki baada ya kupokea ripoti ya kamati ya kuchunguza mchakato mzima wa utolewaji wa Mikopo hii,hali siyo nzuri na nimeona ni vyema tukutane,tushauriane na kuchukua hatua lengo hizi fedha zirudi katka mzunguko"


 Mkuu wa Mkoa Mhe Gabriel ameagiza Watumishi wote wa Halmashauri hiyo wanaohusika kuratibu Mikopo hiyo wahakikishe waliowakopesha wamerejesha ili walengwa ambao ni Wanawake,Vijana na Watu wenye Ulemavu wanufaike na fedha hizo ambalo ni lengo la Serikali.


"Zaidi ya Shilingi Bilioni 3 kutolewa nje ya utaratibu ni nyingi sana,hizo siyo fedha za sadaka ni lazima zirudi,haiwezekani Vikundi vingine vilivyopewa Mikopo ni vya Wanawake lakini ndani yake kuna Wanaume huu ni uchotaji wa wazi wazi wa fedha za Serikali"


Amesisitiza Vikundi vyote 680 vilivyopata Mikopo hiyo Wilayani Nyamagana vifuatiliwe na taarifa zao zijulikane baada ya ripoti kuonesha ni Vikundi 156 pekee ndiyo taarifa zake zimepatikana.


Aidha Mkuu huyo wa Mkoa ameruhusu kuanzia sasa mchakato wa utolewaji wa Mikopo hiyo uendelee baada ya kusimamisha kwa muda wa mwezi mmoja ili kurekebisha kasoro zilizojitokeza kwenye Halmashauri zote za Mkoa wa Mwanza.


Kikao hicho kimewajumuisha Viongozi mbalimbali kutoka Halmashauri ya Jiji la Mwanza wakiwemo Watumishi wa Idara za Fedha na Mipango,Kamati ya Ulinzi na Usalama, na Idara ya Maendeleo ya Jamii na Biashara kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.