• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC Mwanza awataka Maafisa Rasilimali Watu kufanya kazi kwa Weledi

Posted on: June 11th, 2022

_Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe Mhandisi Robert Gabriel ametoa wito kwa Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala walioko kwenye Serikali kuu, Mamlaka za Serikali za Mitaa, Mashirika ya Umma, Wakala na Taasisi binafsi nchini kuhudhuria Mkutano Mkuu wa Pili wa Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala utakaofanyika tarehe 15-17 Juni, 2022.

Amesema hayo leo Juni 11, 2022 wakati wa mkutano na Waandishi wa Habari kwa kushirikiana na kamati tendaji ya umoja wa Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala Tanzania ambapo amefafanua kuwa Mkutano huo utafanyika kwenye ukumbi wa Hoteli ya Gold Crest Jijini Mwanza.


Mhe. Mkuu wa Mkoa amefafanua kuwa umoja huo ulioanzishwa na kusajiriwa Februari 13, 2018 nchini umesaidia kuwaunganisha Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala kwa lengo la Kubadilishana uzoefu na kuishuri Serikali juu ya namna bora ya usimamizi wa watumishi wa Umma na Sekta binafsi.


Vilevile, Mkuu wa Mkoa amewapongeza Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala kwa kukutana Mkoani humo huku akibainisha kuwa itasaidia kuongeza ari ya kuchapa kazi na kuonyana kuhusu utendaji kazi wa kuzingatia Weledi wenye tija.


"Uwepo wa Maafisa Rasilimaliwatu na Utawala zaidi ya 400 hapa jijini ni fursa kwa wafanyabiashara na wadau wa maendeleo na itawapa fursa Maafisa hao kutembelea na kujifunza kwenye vivutio vya kitalii na fursa zilizopo Mkoani Mwanza", amesema.


Mhe Mkuu wa Mkoa amewahakikishia Maafisa hao usalama na amejinasibu  hali ya hewa ni tulivu Jijini humo, uwepo wa vyakula bora na amewakaribisha kushiriki kwenye utambulisho rasmi wa Filamu ya Royal Tour itakayofanyika kwenye viwanja vya Rock City Mall siku ya tarehe 18, Juni 2022.


_Mwisho_

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.