• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC MWANZA AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUJISAJILI NA KUCHUKUA VITAMBULISHO VYA NIDA

Posted on: February 19th, 2024

RC MWANZA AWATAKA WANANCHI KUENDELEA KUJISAJILI NA KUCHUKUA VITAMBULISHO VYA NIDA


*Asisitiza weledi na Uzalendo kwa Mamlaka kwenye Utambuzi na Usajili wa wananchi*


*Atoa wito kwa wananchi kutunza vitambulisho na kuvitumia kwa mujibu wa sheria*


*Ametoa rai kwa Mamlaka hiyo kuandikisha makundi yenye Uhitaji Maalum*


Katibu Tawala Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Jumatatu Februari 19, 2024 amezindua ugawaji wa Vitambulisho vya Taifa (NIDA) kwa wananchi kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo na akatumia hafla hiyo kuwataka wananchi kufika kwenye vituo kujisajili na walivyojiandikisha kwenda wakachukue kadi zao kwani zipo tayari.

Balandya amebainisha kuwa tayari NIDA imekamilisha uzalishaji wa Vitambulisho kwa wananchi wapatao 716, 245 na kwamba vingi bado vipo kwenye Ofisi za Serikali za Mitaa na huku wananchi wakiwa na namba tu za kuwatambua jambo ambalo si sahihi hivyo ni wakati sasa wa kuvichukua kwa ajili ya rejea mbalimbali.

Balandya amesisitiza weledi na uzalendo kwa Mamlaka kwenye Utambuzi na Usajili wa wananchi ili waandikishwe wenye sifa kwa mujibu wa sheria na si vinginevyo na kwamba kwenye utekelezaji wa zoezi hilo wasiliache kundi la watu wenye mahitaji maalum

Vilevile, Katibu Tawala ametoa wito kwa wananchi kutunza vitambulisho na kuvitumia kwa mujibu wa sheria na sio kwa matukio ya uvunjifu wa amani au kutenda makosa ya jinai.

Afisa Usajili wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mwanza Ndugu Daud Hashim Abdallah ametoa wito kwa wananchi kuchangamkia fursa hiyo kwani  kigezo kikubwa cha utambuzi na usajili ni kwa raia kuwa na Miaka 18 na kwamba Mamlaka hiyo imesajili asilimia 84 ya wenye sifa mkoani Mwanza na zoezi hilo ni endelevu.

Vilevile, ametaja changamoto kadhaa zinazowakabili Mamlaka hiyo kwenye zoezi hilo katika usajili na utambuzi wa wananchi ikiwemo muitikio mdogo wa wananchi katika kuchukua vitambulisho na kupelekea mlundikano wa vitambulisho kwenye ofisi za Serikali za mitaa na vijiji.

"Elimu kupitia vyombo vya habari imeendelea kutolewa na mamlaka kwenye redio na vyombo vingine kuhamasisha umma juu ya umuhimu wa kusajiliwa, kutambuliwa na kuchukua vitambulisho kwenye ofisi za Serikali za mitaa." Amesisitiza Ndugu Abdallah.

Aidha, bwana Abdalah ametaja pia changamoto za wananchi kujisajili zaidi ya mara moja na akatumia wasaa huo kuwataka kuwa na viambata muhimu kwa ajili ya usajili.

Jisajili, tukutambue tukutambulishe.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.