• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RC - Mwanza azindua wiki ya Huduma za Maabara Uwanja wa Furahisha

Posted on: May 2nd, 2022

 Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Mhandisi Robert Gabriel, amewaagiza wanasayansi wa Maabara za afya mkoani humo kuongeza usimamizi wa ubora wa vipimo mbalimbali katika maabara zote za serikali na binafsi  ili kujihakikishia huduma bora.

Mhe. Mhandisi Gabriel pia amewataka wataalamu hao kuongeza kasi ya ukusanyaji wa damu kwa ajili ya kutosheleza mahitaji ya damu kwa wahitaji wote.

Mhandisi Gabriel ametoa maagizo hayo leo Mai, 2 wakati akifungua maadhimisho ya wiki ya wataalamu wa maabara za afya kimkoa yanayofanyika uwanja wa furahisha hadi Mei , 6 mwaka huu kwa uratibu wa Chama cha Wanasayansi wa Maabara za Afya (MeLSAT)mkoani humo.

"Niwatake  wataalamu wa afya mfanye kazi kama timu  na kutumia majibu ya maabara (takwimu), muweke mipango endelevu itakayowasaidia kukabiliana na changamoto mbalimbal,"amesema na kuongeza

"Ukusanyaji wa damu umeendelea kufanyika kwa mafanikio  ya kiasi cha kufikia asilimia 69 ya malengo ya kukusanya  chupa za damu 32,173 kwa mwaka.

Naye Makamu wa Rais MeLSAT, Taifa, Joseph Gimbuya, amesema  ili kuboresha afya za watanzania mkazo wa kwanza uwe katika kinga na wa pili katika tiba.

"Lakini tiba isiyo  na uchunguzi sahihi wa kiini na aina ya ugonjwa ni kazi bure  na huongeza gharama kwa mgonjwa, serikali na taifa kwa ujumla.

" Hivyo tunapotafakari matibabu  sahihi yenye gharama nafuu zaidi, matumizi ya maabara ni lazima kwa tabibu ama daktari maana kufanya kazi bila maabara ni sawa na kupiga Ramli au kuwa mganga wa kienyeji,"amesema Gimbuya.

Naye Mwenyekiti wa MeLSAT Mkoa wa Mwanza,  Betrand Msemwa, amesema wanachama wote  wana ari ya kuwahudumia wananchi wakishirikiana na wanataaluma wengine ili kuhakikisha afya za wananchi zinazidi kuwa bora.

Kwa upande wake Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Dkt. Thomas Rutachunzibwa, ametoa wito kwa wataalamu wa maabara kuendelea kufanya kazi kwa weledi na kuwataka washirikiane ili kulinda taaluma hiyo ili  isichafuliwe na watu wachache wenye nia ovu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.