• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

RMO MWANZA APOKEA TELEVISHENI 57, KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA KWENYE VITUO VYA AFYA

Posted on: February 7th, 2024

RMO MWANZA APOKEA TELEVISHENI 57, KUIMARISHA UTOAJI WA HUDUMA KWENYE VITUO VYA AFYA


Mganga Mkuu Mkoa wa Mwanza Thomas Rutachunzibwa amepokea Televisheni 57 Kutoka Wizara ya afya kwa lengo la kutoa taarifa na kusaidia utoaji wa huduma bora kwenye vituo vya afya mkoani humo.

Makabidhiano hayo yamefanyika leo Februari 07, 2024 kwenye ukumbi wa Ofisi ya mkuu wa mkoa ukiwakutanisha Wawakilishi kutoka Wizara hiyo, TAMISEMI na Wakala wa Nishati Vijijini (REA).

"Tunategemea kuwa hizi televisheni zitaeneza ujumbe ambazo wagonjwa pamoja na watumiaji wa vituo vyetu watakuwa wanavifuatilia wakipata mafunzo mbalimbali kutoka kwenye mada mbalimbali ambazo zinahusiana na masuala ya afya" Mganga Mkuu.

Dkt. Rutachunzibwa ametumia wasaa huo kuwataka wananchi na jamii kwa ujumla kuchukua tahadhari za kuepukana na Ugonjwa hatari wa Kipindupindu.

Mwakilishi wa Wakala wa Nishati Vijijini (REA) Jaina Msuya amesema lengo la Mradi huo ni kupeleka umeme kwenye vituo vya afya na pampu za maji vijijini ambao unafikia vituo vya afya 57 nchi mzima pamoja na pampu za maji 363 ambazo zimesambaa kwenye mikoa mbalimbali ya Tanzania kwa gharama ya mradi ni billion 37.4.

"Lengo la kuanzisha huu mradi ni kuwawezesha wananchi wanaokaa maeneo ya vijijini waweze kupata huduma kwa haraka na muda sahihi." Amefafanua.

Pia amewataka wananchi kutumia maji ambayo ni safi na salama yawasaidie katika matumizi yao ya kila siku kwa sababu yatawasaidia kuwalinda na kutunza afya zao,  na itapunguza  kero ya kutafuta maji kwa umbali mrefu hasa kina mama na kuweza kupata muda wa kushiriki kwenye majukumuu mengine kama ya kifamilia.

Mwakilishii kutoka Wizara ya afya James Mhilu ameishukuru wakala wa nishati vijijini (REA) pia ameongeza kwa kuelezea  namna gani mradi huo unaenda kuwasaidia wananchi moja kwa moja, uhakika wa maji na vituo vya kutolea huduma za afya  kupata umeme na kuhakikisha kuwa huduma ya chanzo itaimarika ili kuweza kupambana na magojwa ya mlipuko kama kipindupindu na kuwataka watu wazingatie unawaji wa mikono kwa maji safi na sabuni ili kuepukana na magonjwa, lakini pia mradi huu unaenda kuongeza ufanisi wa utendaji kazi katika vituo vya afya.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.