• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI INAKAMILISHA TARATIBU ZA KUMPATA MKANDARASI WA UJENZI WA BARABARA SENGEREMA-NYEHUNGE : RC MTANDA

Posted on: June 10th, 2024

SERIKALI INAKAMILISHA TARATIBU ZA KUMPATA MKANDARASI WA UJENZI WA BARABARA SENGEREMA-NYEHUNGE : RC MTANDA


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amewataka wananchi wa Wilaya ya Sengerema kuwa na subira wakati Serikali ikikamilisha taratibu za kumpata mkandarasi wa kujenga barabara ya Sengerema -Nyehunge kwa kiwango cha lami.

Amebainisha hayo leo Juni 10, 2024 wakati akizungumza na wananchi wa wilaya hiyo katika mkutano wa hadhara uliofanyika kwenye viwanja vya stendi ya zamani vilivyopo katikati ya mji huo ambapo ulikua wa muitikio mkubwa wa wananchi waliokua na kiu ya kumsikiliza kiongozi huyo wa Mkoa.

Amesema, awali Serikali ilitangaza kazi ya ujenzi wa barabara hiyo

yenye umbali wa takribani KM 50 na kwamba alipatikana mjenzi ambaye alitumia vyeti vya kughushi na kusababisha kupewa kazi wakati hakuwa na uwezo wa kutekeleza na kupelekea Serikali kuwaondoa na iko mbioni kuwachukulia hatua kwa udanganyifu.

"Serikali inayo nia ya dhati ya kujenga barabara ya Sengerema hadi Nyehunge kwa kiwango cha lami na sasa ipo kwenye mchakato wa kumpata mkandarasi mzuri wa kufanya mradi huo baada ya kumuondoa aliyepatikana awali ambaye amebainika kutokua na uwezo"

Vilevile, amewataka vijana kuchapa kazi na kuacha tabia ya kuketi kwenye vijiwe kwani wanasababisha kulirudisha nyuma Taifa kimaendeleo na badala yake wanapaswa kujibidiisha kujitafutia maendeleo kwa kufanya shughuli halali.

Vilevile, Mhe. Mtanda amemuagiza Mkuu wa Wilaya hiyo ndani ya siku 14 kumlipa fidia Bi. Salome Kazungu ambaye mwaka 2017 Halmashauri ililitwaa eneo lake ili kulitumia kama eneo la kuzikana na endapo watashindwa kufanya hivyo atalirejesha kwa mmiliki huyo kwani hajapata haki yake kwa mujibu wa sheria ya ardhi na akatumia wasaa huo kuwataka sekta ya ardhi kushughulikia kero na migogoro.

Mhe. Hamis Tabasam, Mbunge wa Sengerema ametumia jukwaa hilo kumpongeza Rais Samia kwa kuwaletea miradi lukuki ya maendeleo huku akibanisha kuwa kwa sasa kuna shule za Msingi kwenye kila Kijiji na kwamba huduma za maji safi zimeimarika.

Aidha, Mhe. Tabasam amesema kuhusu mikopo kwa wananchi kutoka kwenye fungu la asilimia kumi kutoka fedha za mapato ya ndani tayari zimetengwa zaidi ya Shilingi milioni 300 ambazo zinasubiri utaratibu tu kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu ili zianze kukopeshwa kwa makundi husika.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.