• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI KUJENGA HOSPITALI YENYE HADHI YA MKOA WILAYANI UKEREWE

Posted on: December 27th, 2024

SERIKALI KUJENGA HOSPITALI YENYE HADHI YA MKOA WILAYANI UKEREWE


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amemshukuru Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa uboreshaji wa sekta ya afya mkoani humo hususani ujenzi wa miundombinu bora na ufungaji wa vifaa vya kisasa katika vituo vya kutolea huduma.

Mhe. Mtanda amebainisha hayo leo tarehe 27 Desemba, 2024 katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa Hospitali ya Rufaa yenye hadhi ya Mkoa itakayojengwa katika kijiji cha Bulamba kata ya Bukindo kwa thamani ya zaidi ya Bilioni 25.

Ameongeza kuwa ndani ya muda mfupi Serikali imepeleka Mkoani humo zaidi ya Tshs. Bilioni 49.4 kwa ajili ya uboreshaji wa huduma za afya na jumla ya Trilioni 5.6 zimepokelewa kwa ajili ya utekelezaji wa miradi katika sekta mbalimbali.

Aidha, amemtaka mkandarasi pamoja na msimamizi yaani Ofisi ya Mkuu wa Mkoa kutekeleza mradi huo kwa wakati kwa mujibu wa mkataba na kwa kuzingatia ubora na amewataka kuanza mara moja ujenzi kwakua tayari Bilioni 6 zimeshatolewa na Serikali.

"Uwepo wa Ujenzi huu utawafanya wananchi wa eneo hili na maeneo ya jirani kukua kiuchumi kutokana na kuongezeka kwa muingiliano wa watu na kufungua fursa kwa sekta zingine kwa kuwekeza jirani na eneo hili, hivyo tunamshukuru sana Mhe. Rais kwa upendo huu." Amesisitiza.

Akielezea mradi huo utakaotekelezwa na kampuni ya M/S DIMETOCLASA REALHOPE LIMITED kwa kipindi cha miezi 18, Katibu Tawala Msaidizi sehemu ya Miundombinu Mkoa wa Mwanza Mhandisi Chagu Ng'oma amesema mradi huo umegawanywa katika awamu 4.

Aidha, ameahidi kusimamia kwa dhati utekelezaji wa mradi huo ambao amefafanua kuwa awamu ya kwanza utahusisha ujenzi wa jengo kuu la hospitali litakalokuwa na uwezo wa kubeba vitanda 180, Ofisi tatu za walinzi, Jengo la kuhifadhia maiti na Jengo la umeme na kazi za nje.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.