• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali kuwachukulia hatua kali Shule na wahusika na udanganyifu wa mitihani ya kidato cha nne mwaka 2022

Posted on: February 19th, 2023


Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Prof.Adolf Mkenda amesema Serikali inaendelea kufanya uchunguzi kwa shule zote nne zilizobainika kufanya udanganyifu wa mitihani ya kidato cha nne mwaka 2022 na wahusika wote watakao bainika watachukuliwa hatua kali za kinidhamu ikiwemo kufukuzwa kazi.

Akizungumza leo kwenye ukumbi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza na wazazi wa wanafunzi 140 wa shule ya Sekondari ya Thaqafa waliofutiwa matokeo yao,Mhe.Mkenda amesema vitendo hivyo havitavumiliwa la kuja kuwa na Taifa la watu wasio na weledi na wasomi wababaishaji.

Kuhusu ombi la wazazi hao la kutaka watoto wao kurudia mitihani,Waziri Mkenda amesema kwa sasa hawezi kuwa na jibu la moja kwa moja kutokana na suala hilo kuwa la kibajeti zaidi na Baraza la Mitihani la Taifa halina fungu hilo kwa sasa hivyo wampe muda wa kuzungumza na wasaidizi wake Wizarani na baadaye Serikali itakuwa na jibu la kuwapa.

Aidha amewashauri wazazi wanaowasomesha watoto wao kwenye shule hizo nne ambazo ni Mnemonic ya Zanzibar,Thaqafa kutoka Mwanza,Cornelius ya Dar  es Salaam,na Twibhoki kutoka Mara wajitathmini kama watoto wao wanastahili kuendelea kusoma kwenye shule hizo kabla ya hatua za kinidhamu hazijachukuliwa na Serikali.

"Wazazi wenzangu awali ya yote poleni sana, natambua mlivyo umizwa na jambo hili,Kamishna wa Elimu Dkt.Lyabwene Mutahaba na timu yake wapo katika hatua za uchunguzi kwa shule hizo na hatua itakayofuatia ni kuzifutia usajili ili iwe fundisho kwa wengine wanaojihusisha na mmomonyoko huo wa maadili" Prof.Adolph Mkenda.

Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe.Adam Malima amewataka wazazi hao kukaa chini na watoto wao ili wawaambie ukweli mienendo ya walimu wao kutokana na kuendelea mambo ya ovyo sana huko shuleni vikiwemo vitendo vya Uzalilishaji kijinsia na ngono.

"Ofisi yangu na Idara ya Elimu ipo wazi kupokea taarifa yoyote inayohusiana na matendo ya ovyo yanayofanywa na baadhi ya walimu wasio na maadili yakiwemo udanganyifu wa mtihani na ngono sitakuwa na huruma kwa watakaobainika zaidi ya kuwafikisha kwenye vyombo vya dola"Mkuu wa Mkoa.

"Mhe.Waziri tunaamimi nawe ni mzazi tumeguswa sana na udanganyifu huu uliofanyika ambao umeingia kutugharimu sisi wazazi, tunakuomba sana utufutie machungu haya kwa kuwaruhusu watoto wetu kurudia mitihani yao" Patrick Masagati Mwenyekiti wa Wazazi shule ya Thaqafa.

Jumla ya wanafunzi 162 walifanya mtihani wa kumaliza kidato cha nne shule ya Sekondari Thaqafa mwaka 2022 na wanafunzi 22 matokeo yao yalitoka na 140 kufutiwa baada ya kubainika kufanya udanganyifu.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.