Swahili
  • English
  • Swahili
    • Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

Posted on: May 1st, 2025

SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA


Serikali mkoani Mwanza imesema Katika kipindi cha mwaka 2023/2024 na 2024/2025 Sekretarieti ya Mkoa na Halmashauri zake nane zimepata mafanikio makubwa katika kuhakikisha kwamba masuala ambayo ni kero kubwa kwa watumishi yamefanyiwa kazi kwa kiasi kikubwa.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda katika Maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi duniani yaliyofanyika Kimkoa katika Viwanja vya KWIDECO Wilayani Kwimba ambapo amesema Serikali imelipa watumishi 3,556 fedha za malimbikizo ya mishahara (Salary Arreas) yenye jumla ya shilingi 6,896,355,330/= na Watumishi wapya 831 wameajiriwa ili kupunguzia mzigo kwa watumishi.

Aidha, Mkuu wa Mkoa amesema Serikali imelipa madai ya watumishi 4,015 yasiyo ya mshahara (mfano likizo, matibabu uhamisho n.k) yenye kiasi cha Shilingi 3,283,016,595,486/=.

“Si hayo tu bali pia Watumishi 9,829 wa kada mbalimbali wamepandishwa madaraja (vyeo) kwa mwaka wa fedha 2023/2024 na watumishi 601 wamebadilishiwa kada (Recategorization) kwa mwaka wa fedha 2023/2024”.

Kadhalika Watumishi wameendelea kupewa fursa za kujiendeleza ambapo hadi kufikia mwezi Aprili, 2025 jumla ya watumishi 528 wapo masomoni katika Vyuo mbalimbali. Watumishi 1,352 wameajiriwa katika sekta mbalimbali ndani ya Mkoa wa Mwanza. Amesema Mhe. Mtanda akiendelea kuelezea mafanikio hayo.

Mkuu wa Mkoa ameendelea kwa kusema Utekelezaji wa Mfumo wa Usimamizi wa Utendaji Kazi katika Utumishi wa Umma (PEPMIS) kwa mwaka wa fedha 2024/2025, umefikia asilimia 59.72 huku Mfumo huo ukiwa na lengo la kuimarisha uwajibikaji na utendaji kazi unaojali matokeo katika Utumishi wa Umma ili kuwaletea wananchi maendeleo.

Kuhusu suala ya Ajira kwa Vijana Mkuu wa Mkoa amesema Jumla vikundi 37 vya vijana hadi sasa vimewezeshwa miundombinu ili kufuga Samaki kwenye vizimba 161 ndani ya ziwa Victoria hivyo

kupunguza changamoto ya ajira kwa vijana wa Mkoa wa Mwanza.

“Miradi ya Kimkakati imezalisha ajira mbalimbali kama vile Ujenzi wa madarasa na ujenzi wa miundombinu mingine ya Utawala, Elimu na Afya ulizalisha ajira 15,855, Ujenzi wa Meli Mpya ya MV Mwanza Hapa Kazi tu umezalisha ajira 1,000, Ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR umezalisha ajira 3,075, Ujenzi wa daraja la JPM umezalisha ajira 1,875 Huku Ajira 2,758 zimezalishwa kupitia fedha za Mfuko wa Vijana, Wanawake na Watu wenye Ulememavu.”.

Mkuu wa Mkoa amesema kwa kufafanua mafanikio hayo ni kuwafanya Wafanyakazi hao waweze kupata picha halisi ya mafanikio makubwa na ya kupigiwa mfano yaliyopatikana kwenye upande wa watumishi katika Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • RAS MWANZA AWATAKA VIONGOZI WA UMMA KUDUMISHA NIDHAMU NA UFANISI KAZINI

    May 26, 2025
  • FAMILIA NI NGUZO IMARA KATIKA KULINDA MAKUZI YA MTOTO: DKT. BITEKO

    May 24, 2025
  • RC MTANDA AIPONGEZA BENKI YA NCBA KWA KUWAENZI WATEJA WAKE

    May 23, 2025
  • RC MTANDA AKABIDHI MAGARI MAWILI KWA MA-DC UKEREWE NA MAGU.

    May 23, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.