• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali yaipongeza Kampuni ya Huduma za Meli Kwa ujenzi unaoridhisha wa MV Mwanza

Posted on: January 17th, 2023


Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Makame Mbarawa (MB) amewapongeza Kampuni ya Huduma za Meli (MSCL) kwa Utekelezaji unaoridhisha wa Mradi wa Ujenzi wa Meli ya Kisasa ya MV Mwanza inayojengwa kwa gharama ya Bilioni 108 itakapokamilika.

Prof. Mbarawa amesema hayo leo (Januari 17, 2023) alipofanya ziara kwenye bandari ya Mwanza Kusini ambapo Meli hiyo inajengwa na kukuta Ujenzi umefikia Asilimia 80 ya Utekelezaji.

Amesema Wizara hiyo imeridhika na utekelezaji wa mradi huo na akabainisha kuwa ifikapo februari 15 mwaka huu meli itaondolewa kwenye chelezo na kuingizwa kwenye Maji ambapo Ujenzi wa hatua zilizobaki utaendelea ikiwa majini.

"Ujenzi unaenda vizuri na Serikali tumeridhika na hatua zote na ifikapo tarehe 15 mwezi ujao  (februari) meli hii itaingizwa kwenye Maji kwa ajili kuendelea na ujenzi wa hatua zinazofuata za ukamilishaji." Mhe. Mbarawa.

Aidha, amewaagiza Kampuni ya Huduma za Meli kufuatilia kwa kina ufungaji wa vifaa vya kumsaidia Nahodha kuweza kubaini mahali gani pana hali gani kama vile kina kidogo au miamba (Navigation Chat).

Vilevile, amewataka MSCL kusimamia Ujenzi wa Bandari ya Kemondo (Kagera) ili ikamilishwe kwa haraka na kuhakikisha anapatikana mkandarasi wa kujenga Bandari ya Mwanza kusini ili Meli hiyo ianze kazi mara moja bila kusubiri jambo lolote.

Naye, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Adam Malima ameipongeza Wizara hiyo kwa kazi nzuri wanazoendelea kusimamia huku akiitaja Miradi ya kimkakati ya Reli ya Kisasa, Daraja la Kigongo-Busisi na Meli hiyo ambayo yote kwa pamoja itawainua sana wananchi wa Mwanza na Tanzania kwa ujumla.

Aidha, Mhe. Malima ametoa wito kwa MSCL kujifunza kwenye Bandari kubwa za kimataifa ili kuhakikisha wanajenga bandari za kisasa zitakazoendana na Meli hiyo inayotarajiwa kuwanufaisha watanzania na nchi za jirani.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.