• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SERIKALI YATOA BILIONI 56 KUIMARISHA USAFIRI WA VIVUKO NCHINI: WAZIRI ULEGA

Posted on: January 24th, 2025

SERIKALI YATOA BILIONI 56 KUIMARISHA USAFIRI WA VIVUKO NCHINI: WAZIRI ULEGA


Serikali imetoa jumla ya Tshs. bilioni 56 ili kuimarisha usafiri wa Vivuko 6, vitano vinakamilishwa Mwanza na kimoja Mafia mkoani Pwani lengo likiwa kuwaondolea adha ya usafiri wa maji wananchi wa maeneo ya visiwani.

Akizungumza mapema leo Januari 24, 2025 kwenye karakana ya Songoro wilayani Ilemela mkoani Mwanza vinapojengwa Vivuko 5 kwa gharama ya Tshs bilioni 21,Waziri wa Ujenzi Mhe. Abdallah Ulega (MB) ambaye yupo ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa miundombinu amebainisha tayari Serikali imetoa Tshs. bilioni 45 kuwalipa wakandarasi wanaodai kwenye miradi ili kuhakikisha kazi hizo zinakamilka kwa wakati.

"Nafurahi kuona maendeleo mazuri ya ujenzi wa Vivuko hivi, tayari siku ya jana nimeidhinisha fedha sasa ni imani yangu mkandarasi Songoro Marine kazi ya umaliziaji itakwenda vizuri", Waziri Ulega.

Amefafanua kuwa fedha hizo bilioni 56 ni pamoja na gharama ya Vivuko hivyo 6 ambayo ni shs bilioni 32.2 na fedha inayobaki ni gharama ya ukarabati wa Vivuko vya MV Kigamboni, MV Magogoni na MV Nyerere.

Kwa upande wake Meneja wa karakana hiyo Meja Songoro amesema vivuko hivyo vitano vipo katika hatua za mwishoni na kuishukuru Serikali kwa ushirikiano mzuri",Songoro.

Aidha, Waziri Ulega ametoa maelekezo kwa Wakala wa ufundi na umeme,Tamesa wanaosimamia Vivuko hivyo kuhakikisha wanafanya usimamizi mzuri ili vyombo hivyo vya usafiri viwe na tija kwa wananchi.

Akiwa kwenye ukaguzi wa daraja la JP Magufuli lenye urefu wa km 3 na barabara unganishi ya km 1.66 lenye thamani ya zaidi ya shs bilioni 700, Waziri Ulega amesema tayari ameidhinisha malipo ya shs bilioni 16 kwa mkandarasi CCEC ili aweze kulikamilisha kama walivyokubaliana na Serikali Februari 28,2025.

"Mhe. Waziri daraja hili mbali ya kujengwa kitaalamu wa hali ya juu na kuwa daraja refu kwa nchi za Afrika Mashariki, pia litadumu kwa miaka 100 na sasa lipo katika hatua ya uwekeji lami",Mhandisi Dorothy Mtenga, Kaimu Mtendaji Mkuu, TANROADS.

Mhe. Abdallah Ulega hii ni ziara yake ya kwanza mkoani Mwanza akiwa Waziri wa Ujenzi akitokea  Wizara ya Uvuvi na Mifugo aliyohamishiwa mwishoni mwa mwaka jana

.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.