• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Serikali yawahimiza vijana kuchangamkia fursa za mazingira ya kujiajiri wanayoandaliwa

Posted on: July 19th, 2023

Serikali yawahimiza vijana kuchangamkia fursa za mazingira ya kujiajiri wanayoandaliwa.


Serikali imeendelea kuwahimiza vijana kuchangamkia fursa za kujiajiri wakati wakiandaliwa mazingira mazuri ya kumudu hatua hiyo.

Waziri wa Mifugo na Uvuvi Mhe.Abdallah Ulega ametoa kauli hiyo jumanne hii huko Wilayani Misungwi kwenye Shamba

la Taifa la Mifugo wakati wa hafla fupi ya kupokea Lori la Tani 10 na Pikipiki 4 kwa ajili ya mradi wa vijana wanaojihusisha na unenepeshaji mifugo,kiongozi huyo mwandamizi wa Serikali amesema Serikali inatambua mchango wa vijana katika ujenzi wa Taifa hivyo wasikate tamaa.

"Leo napokea msaada huu kwa niaba yenu kutoka marafiki zetu wa maendeleo Shirika lisilo la Kiserikali la Heifer International,hizi ni juhudi zinazofanywa kuhakikisha hampotezi muda wenu hapa badala yake mtoke hapa mkiwa ni wataalam wa uhakika,"Abdallah Ulega,Waziri wa Mifugo na Uvuvi

Mhe. Ulega amebainisha anatambua sekta ya mifugo na Uvuvi ni ya uzalishaji hivyo ni jukumu lao kama Wizara kuendana na maono ya Rais Dkt.Samia kulikomboa kundi kubwa la vijana na kuingia katika hatua ya kujiajiri baada ya kuandaliwa kisasa.

Amewataka vijana hao kutokata tamaa kwani siku zote mambo mazuri hayaji kirahisi ni lazima kupitia changamoto za hapa na pale kufikia mafanikio mazuri.

"Sisi kama Mkoa tumejipanga kuhakikisha malengo yote mazuri kwa vijana yanakuja na matokeo chanya kwa kusimamia na kufuatilia kikamilifu",Emil Kasagara,Katibu Tawala Msaidizi Uchumi na Uzalishaji.

"Tunatambua hatari ya kuliwacha kundi la vijana ambao ni nguvu kazi ya Taifa,sisi kama Heifer International tupo bega kwa bega na Serikali kufikia malengo yaliyo kusudiwa,"Mark Tsoxo,Mkurugenzi mkazi Heifer International.

"Tunaishukuru Serikali ya Rais Samia kwa juhudi za kutuendeleza sisi vijana,mradi huu wa unenepeshaji mifugo utakuwa ni mkombozi kwetu na kuzidi kuiborsha Sekta ya mifugo nchini," Suzana John mnufaika na mradi wa viatamizi.  

Jumla ya vijana 900 wapo kwenye Shamba la Taifa la Mifugo wakiendelea kupata mafunzo ya kisasa ya ufugaji wa kisasa ambapo kila mmoja amekabidhiwa ng'ombe 10 kumfuga kisasa na kumuuza na baadaye kujipatia mtaji wa kujiendeleza.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.