• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Siku ya Ukimwi Duniani,Rai yatolewa Mwanza kuepukana na tabia hatarishi

Posted on: December 1st, 2022


Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Adam Malima ameiasa jamii kuachana na tabia hatarishi zinazochochea Maambikizi ya VVU/UKIMWI ili kuepukana na athari za janga hilo.

Malima ametoa rai hiyo leo (Disemba 01, 2022) kwenye viwanja vya Mirongo Jijini Mwanza wakati wa Maadhimisho ya Siku ya UKIMWI duniani yaliyofanyika kimkoa kwenye viwanja hivyo.

"Kwa takwimu hizi za Maambukizi ya Asilimia 7.2 Mkoani kwetu ambayo ni zaidi ya Asilimia 4 ya Kitaifa inaonesha hali ya Maambukizi kwa Mwanza kuwa bado yapo juu sana hivyo ni lazima tulifanyie kazi suala hili hususani kuwakinga na janga hili watoto wetu ambao ni Taifa la kesho." Malima.

Aidha, ametoa wito kwa wenye Maambukizi ya VVU/UKIMWI kutumia dawa za kufubaza maambukizi ili kuendelea kuzalisha uchumi wao kwa kujitafutia kipato kwa kukuza  mitaji inayosaidia kuboresha maisha yao.

Hata hivyo, ametoa wito kwa mashirika yote Mkoani humo kushirikiana na serikali katika kukidhi matakwa ya kitaalamu na miongozo ya Wizara ya Afya katika kuhudumia Wananchi na amezitaka Halmashauri kupeleka nguvu kwenye afua za kudhibiti maambukizi ya VVU/UKIMWI.

Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi Mkazi wa ICAP nchini ndugu Michael Kalunga amesema shirika hilo linaendelea kushirikiana na Serikali kupitia kutoa msaada wa vifaa tiba kuhakikisha wanafikia malengo ya kusaidia watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi waweze kufahamu hali zao.

Yasin Ally, Mkurugenzi wa Shirika la Kivulini amesema Shirika hilo linafanya jitihada katika kuhakikisha wanakemea masuala ya ukatili wa kijinsia kama Ubakaji wenye matukio  479, matukio 1115 ya Mimba za utotoni na 1044 ya Ulawiti mkoani humo ili kuwafanya watoto waweze kustawi.

Akisoma risala ya Maadhimisho hayo, Joseph Kiarata amesema huduma zisizo na vikwazo kwa watoto na jamii kwa ujumla ndiyo lengo la Serikali katika kuhakikisha wananchi wanapata huduma za kijamii bila ubaguzi.

"Katika 2016 hadi 17 Mkoa wa Mwanza uliongeza maambikizi ya VVU/UKIMWI kwa asilimia 7 lakini Serikali inaendelea kufanya afua mbalimbali za kusaidia kufuta maambukizi mapya kama matumizi ya kondomu, kukemea matumizi ya dawa za kulevya, ndoa za utotoni, ulawiti na Ubakaji na kuhudumia wanaoishi na VVU/UKIMWI.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.