• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SUMATRA Yawabana Leseni Feki,Vishoka

Posted on: August 8th, 2018

Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi kavu(SUMATRA) imefanya mkutano  kati yao na wamiliki wa magari pamoja na madereva wa  magari katika Ofisi ya Mkuu wa Mkoa Mwanza, kwa ajiri ya kutatua changamoto za usafirishaji wa barabarani na kutoa elimu ya maombi ya leseni kwa njia ya mtandao.

Mkurugenzi Mkuu wa SUMATRA  Bw.Gilliad Ngewe amesema kuwa kazi ya SUMATRA ni kusimamia huduma za usafirishaji wa barabara na majini kwa kufuata sheria,kanuni na utaratibu na kutoa elimu ili kuondoa umiliki wa leseni feki na wasio na  leseni na kuwaondoa vishoka.

"Tutadhibiti  mitandao yote feki ya jutoaji leseni,rushwa na kuwachukulia hatua kali za kisheria kwa wamiliki wote wa leseni feki, pia kwa kuwafungia vifaa maalum vya kudhibiti mwendo kwenye mabasi ya mikoani, kwa ajili ya kuzuia ajari za barabarani, ili kusaidia kupunguza matumizi  makubwa ya mafuta, matumizi ya matairi mabovu na ufungaji wa breki njiani ovyo,"alisema Ngewe.

Kwa upande wake Meneja wa leseni SUMATRA Leo Ngowi ameeleza jinsi ya kuomba leseni kwa njia ya mtandao na kusema kuwa vitu vinavyohitajika kwenye kujaza maombi ya kwa njia ya mtandao ni lazima uwe na Nakala ya kadi ya udereva, Bima ya gari, Nakala ya leseni ya Udereva na Hati ya ukaguzi, kwa kutumia njia hii itasaidia kuondoa leseni feki na kuokoa muda.

Nao wamiliki na madereva wa magari wametoa changamoto zao hasa katika upande wa faini za mara kwa mara za barabarani, kuondoa vishoka, na kuzingatia upande wa walemavu, wawe wanakuja wenyewe SUMATRA barabarani kukagua na kuomba matatizo hayo yarekebishwe na sio kuendelea kuongelewa kila siku bila kufanyiwa marekebisho.

Aidha  Mkaguzi Msaidizi wa Polisi kutoka Ofisi ya Mkuu wa Kitengo cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza Issa Hamad ameekezea juu ya ukaguzi wa leseni na bima kwa njia ya mtandao.

 "Endapo akiingiza namba ya bima na leseni yako kama ni feki au imeisha muda wake mfumo huwa unasema na matokeo yake unatakiwa kwenda kulipa faini  pia muda mwingine tunakukagua gari lako pasipo kukuambia ila tukigundua kama unakosa huwa tunakulipisha faini na kukupa risiti ukalipie kwa kukwepa malumbano ya kuanza kukuelezea kosa tutachukua mda mrefu,"alisema Hamad.

Mkuu  wa Kitengo cha Usalama Barabarani Mkoa wa Mwanza  ACP M.K. Mkadam amesema anahitaji wampelekee magari ya polisi yanayofanya makosa, anahitaji watendaji wake wafanye kazi na ametoa namba ya simu kwa wananchi kwa ajiri ya kuwashitaki madereva ambao hawafikishi katika vituo wanavyohitaji kushuka, na alisisitiza kutoa elimu zaidi ili waende na wakati.

Hata hivyo Mhe.Ngewe amemalizia kwa kuwataka madereva na wamiliki wa magari wafuate sheria, kanuni na utii ili kuondoa matatizo ya barabarani na waache kutoa rushwa hivyo itasaidia kuondoa leseni feki na vishoka.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.