• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

SUNGUSUNGU DAY YAFANA MWANZA, RAIS SAMIA ASIMIKWA UTEMI

Posted on: June 20th, 2025

SUNGUSUNGU DAY YAFANA MWANZA, RAIS SAMIA ASIMIKWA UTEMI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan leo juni 20, 2025 amezungumza na jeshi la jadi Sungusungu zaidi ya elfu 30 katika viwanja vya CCM Kirumba ambapo amesimikwa Utemi na jeshi hilo kama ishara ya kumuunga mkono katika kulinda amani nchini.

Akizungumza na kundi hilo pamoja na mengine Mhe. Rais amewashukuru kwa kumsimika Utemi na akawataka kuendelea kulinda amani na kwa makundi ya boda boda kufuata sheria za usalama barabarani ili kulinda uhai wa watumiaji barabara kwa kuwaepusha na ajali zinzozuilika.

“Maendeleo yaliyofanyika nchini yanahitaji kulindwa na kutunzwa kama miundombinu ya maji, shule, hospitali, umeme na kwakua ninyi ndio walinzi kwenye jamii naomba tuendelee kuwa msitari wa mbele kwenye kuitunza na nawaomba mkabebe sera za serikali kama chanjo ya mifugo ili wafugaji wakaitumie vema.”

Vilevile, ametoa rai kwa makundi mbalimbali nchinu kuunda vikundi na kurumia fursa za mikopo ya aslimia 10 ili kufanya biashara na kukuza uchumi wao na akawataka maafisa kwenye halmashauri kuwasaidia kufanikisha hilo hususani ujazaji sahihi wa fomu.

Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amempongeza Mhe. Rais kwa kazi kubwa anayoifanya katika kuongoza serikali ya awamu ya sita na amemuahidi kwa niaba ya mikoa ya kanda ya ziwa akiwa mwenyekiti wa wakuu wa Mikoa kuwa jeshi hilo na jadi litalinda amani.

Aidha, pamoja na shukurani hizo Mhe. Mtanda ametumia fursa hiyo kuwasilisha zawadi ya Mkoa wa Mwanza kwa Mhe Rais ambayo ni ng’ombe kumi waliotolewa na makundi mbalimbali

Akitoa salamu za Sungusungu kutoka mikoa ya Shinyanga, Simiyu, Geita, Mara na Mwanza ndugu Richard Bundala amesema wanayo furaha kuazimisha miaka 42 tangu kuanzishwa kwa jeshi hilo la jadi na kwamba wanaendelea kulinda amani ya nchi kwa kuhamasisha jamii kuacha tabia hatarishi kama wizi wa mali.

“Mwanzoni mwa miaka ya 1980 kulishamiri wizi wa mifugo na mali ndipo wazazi wetu wakaanzisha jeshi la jadi lililohakikisha linakomesha kadhia hiyo ambayo tunaendeleza na tunatoa wito kila raia kulinda mali ili kuongeza msukumo wa kujihusisha na uzalishaji maji.” Amesema Bundala.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • KAMA TUNAHITAJI KUSONGA MBELE NI LAZIMA KUJIUNGA NA USHIRIKA – RAS BALANDYA

    June 24, 2025
  • RAS BALANDYA AFUNGUA MAFUNZO YA PEPMIS KWA WATUMISHI WA UMMA

    June 23, 2025
  • SHEREHE ZA BULABO KUPANDISHWA HADHI KUWA URITHI WA UTAMADUNI

    June 21, 2025
  • SUNGUSUNGU DAY YAFANA MWANZA, RAIS SAMIA ASIMIKWA UTEMI

    June 20, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.