• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

Tanzania Yataka mataifa yanayoshiriki maonesho,TCCIA Kujenga viwanda

Posted on: September 18th, 2019


 Serikali imezitaka kampuni kutoka mataifa ya Kenya, Uganda,  China, Egypt na India ambazo zimekuwa zikishiriki maonesho ya Afrika Mashariki yanayoandaliwa na  Chemba ya Wafanyabiashara,wenye Viwanda na Kilimo Tanzania (TCCIA) na yale ya kimataifa ya  Biashara ya Dar es Salaam (DITF) maarufu Sabasaba kujenga viwanda vyao nchini.

Kauli  hiyo imetolewa na Mkurugenzi Mtendaji wa  Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (Tantrade),  Edwin Rutageruka ambaye alimwakilisha Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa katika ufunguzi wa maonyesho ya 14 ya TCCIA yanayofanyika katika viwanja vya jengo la biashara la kimataifa la Rocky City Mall, jijini Mwanza.

Rutageruka amesema  sababu ya Serikali kuzitaka kampuni hizo  kujenga viwanda vyao nchini  kutokana na  bidhaa zao zinakubalika kwa watanzania na zaidi katika kushindanisha washiriki wa maonyesho mbalimbali  zimekuwa zikiibuka na ushindi wa jumla  na kujizolea  vikombe   vingi.

Alisema  hakuna haja ya kampuni hizo kuendelea kupata usumbufu wa kusafirisha bidhaa zao kila mwaka kuleta Tanzania kwa ajili ya maonyesho, hivyo ni wakati muafaka wa kuwekeza nchini kwa kujenga viwanda ikiwa ni sehemu ya uwekezaji kwani tayari soko limepetikana.

“Ninachozungumza hapa ni  cha waziri Bashungwa ambaye anasema wakati Serikali inawakaribisha wawekezaji kutoka mataifa mbalimbali kuja kuwekeza nchini kutokana na bidhaa zao kukubalika, ni wakati muafaka kwa watanzania kujifunza na kuiga kile kinachofanywa na wenzetu, tusiendelee kupenda vya wengine na kusahabu vya kwetu.

“Mimi ni mzoefu katika maonyesho haya ambayo yamekuwa yakifanyika kila mwaka, ukifika katika mabanda ya washiriki wakigeni unakuta watanzania wamefurika pale wakinunua bidhaa zao, mfano kampuni ya Movit ya Uganda inakuwa na wateja wengi, sasa hakuna haja kila mwaka kusafirisha bidhaa, kama Serikali tunawataka waje tuwape maeneo ya kujenga viwanda vyao.

“Tanzania ni salama na inawakaribisha wawekezaji kutoka Kenya, Uganda,  China, Egypt na India kwani hawa kila mwaka wanapata vikombe vya washiriki na bidhaa bora, hata leo sote tumeshuhudia hapa zawadi nyingi zimechukuliwa na kampuni za nje, naomba viwanda vijengwe hapa Mwanza kwani ndio kitovu cha nchi za Afrika Mashariki,”alisema.


Katika hatua nyingine, Rutageruka alisema sekta ya kilimo inaendelea  kukosa mvuto kwa watanzania na  wengi wao wamegeukia biashara ambapo aliwashauri viongozi TCCIA wanaoshughulikia sekta ya kilimo kuendelea kuhamasisha wananchi  kuachana na kilimo cha jembe la mkono na kulima kisasa.


Wakati huo huo,alisema asilimia 70 ya wafanyabiashara wa mipakani ni wanawake ambao wengi wao wanafanya shughuli za kiuchumi zisizo rasmi hivyo aliwataka viongozi wa TCCIA na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kuendelea kuwalimisha  ili kutambulika.


Kwa upande wa Mwenyekiti wa TCCIA Mkoa wa Mwanza, Dkt. Elibariki Mmari alisema changamoto iliyopo kubwa  ni washiriki kutoka nje ya Tanzania kusumbuliwa mipakani wanapotaka kuingiza bidhaa  zao kwa ajili ya maonyesho  hayo  kwani huchukua muda mwingi kuthibitisha bidhaa.


Dkt. Mmari aliendelea kuiomba  Serikali kuwapatia  eneo la Nyamhongolo jijini Mwanza ambalo limekuwa likitumika katika maonyesho ya  wakulima maarufu nane nane ili kuliwekeza  katika hadhi ya kimataifa.


Dkt. Mmari alisema miongoni mwa fursa zitakazopatikana kutokana na maonyesho hayo ni kuimarisha mtandao wa masoko na usambazaji bidhaa,  kampuni za Tanzania kujifunza na kutanua wigo wa biashara kwa kutumia  makubaliano ya kibiashara ya kimataifa.


Vile vile alisema kufanyika maonyesho hayo yanatoa mchango kwa vitendo katika kuunga mkono juhudi za Rais Mhe. Dkt. John Magufuli kuifanya Tanzania ya viwanda na uchumi wa kati ifikipo 2025 sambamba na kuimarisha mtengamano wa soko la pamoja la Afrika Mashariki.





Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.