• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TARURA KILIMANJARO WAJIFUNZA UJENZI WA BARABARA ZA MAWE MWANZA

Posted on: September 6th, 2023

TARURA KILIMANJARO WAJIFUNZA UJENZI WA BARABARA ZA MAWE MWANZA


Leo Septemba 06, 2023 wafanyakazi 25 kutoka Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (TARURA) Mkoa wa Kilimanjaro wamewasili mkoani Mwanza kwa ziara ya siku 1 ya mafunzo ya namna ya kujenga barabara kwa kutumia teknolojia ya mawe hususani kwenye maeneo ya miinuko.

Katibu Tawala Msaidizi Seksheni ya Miundombinu, Mbunifu Majengo Chagu Nghoma amesema Teknolojia hiyo inasaidia kuwafikia wananchi wanaoishi kwenye miinuko kutokana na kuwapelekea barabara ya kudumu kwa gharama nafuu tofauti na siku za nyuma ambapo walijengewa kwa udongo na changarawe na kupelekea kutodumu kwa muda mrefu.

Vilevile, amebainisha kuwa kutokana na kufikika kwenye maeneo hayo kutokana na uwepo wa barabara, inaweka pia mazingira rahisi ya kupeleka huduma za jamii kama Shule, Masoko, Maji na Umeme kwenye makazi ya miinuko kutokana na mipango miji kuwa inayoeleweka tofauti na kwenye makazi ambayo kunakua na barabara za asili zisizopitika kwa urahisi.

"Ujenzi wa barabara hizi unasaidia sana kutumia nguvu kazi za wananchi kwenye eneo husika kwa ajira za muda na inailetea sifa Serikali kwa kutekeleza miradi hiyo kwa kundi kubwa la wananchi wanaoishi kwenye makazi ya miinuko ambao hali zao wengi ni za chini kiuchumi." Amefafanua Nghoma.

Meneja wa TARURA Mkoa wa Mwanza Mhandisi Goodluck Mbaga amesema Teknolojia ya Ujenzi wa barabara za mawe ni nzuri na nafuu kwani kwa barabara ya Kilomita Moja inagharimu wastani wa Milioni 360 tofauti na gharama za kujenga barabara za kiwango cha Lami ambayo hugharimu zaidi ya Milioni 800 kwa Kilomita.

"Teknolojia hii ni nafuu na bora sana yaani inakupa uwezo hata wa kuyatumia mawe hayo kwa shughuli zingine baada ya muda wa barabara kuisha na tunawashukuru sana wetaalamu walioileta teknolojia hii hapa nchini miaka ya 2007 ambapo ilijengwa barabara ya kwanza Kigoma kabla ya mwaka 2008 kuitumia mkoani Mwanza." Mhandisi Mbaga.

Meneja TARURA Kilimanjaro Mhandisi Francis Nicholas amesema ziara yao ina tija kwani wamekuja Mwanza kujifunza namna ya kutumia teknolojia ya ujenzi wa barabara za mawe huku akibainisha kuwa wana maeneo ya miinuko na wana utajiri wa mawe mkoani kwao hivyo wameona waje wajifunze namna ya kutekeleza hususani kuyadhibiti maji.

Amesema kuwa Same na Mwanga ni miongoni mwa wilaya zenye jiografia ya milima na mawe mengi na katika kutimiza adhma ya kumsaidia Mhe. Rais Samia kutekeleza miradi ya barabara kwa gharama za chini lakini kwenye ubora hivyo wameona waangazie kwenye matumizi ya teknolojia hiyo ambayo huzalisha barabara za kudumu muda mrefu.

Awali Mhandisi David Christopher kutokka Ofisi ya Meneja wa TARURA Mwanza alielezea kuwa Mkoa huo una barabara zenye Urefu wa Kilomita 18.74 na kwamba halmashauri ya Jiji la Mwanza ilikua ya kwanza kujenga barabara zenye Urefu wa Kilomita 1.5 Mwaka 2008 kabla ya kuanzishwa kwa TARURA.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.