• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TARURA Yaanza ukusanyaji wa ushuru wa maegesho kwa njia ya kielekitroniki

Posted on: July 20th, 2018


Wamiliki wa magari na madeva jijini Mwanza waliozoea ‘kumalizana’ na wakata ushuru wa maegesho itabidi sasa hawatakuwa na njia zaidi ya kulipa ushuru halali baada ya shughuli hiyo kukabidhiwa kwa Wakala wa Barabara za Mijini na Vijijini (Tarura).

Baada ya kukabidhiwa kazi hiyo ambayo awali ilifanywa kwa uwakala kati ya kampuni binafsi na halmashauri, Tarura imetangaza kuanzisha mfumo wa kielektroniki utakaolipiwa moja kwa moja kwa njia ya mtandao.

Akizungumza wakati wa kikao cha wadau wa barabara jijini Mwanza leo Julai 20, Mratibu Tarura Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Koyoya Fuko amesema mfumo huo utaanza kufanya kazi miezi mitatu kuanzia sasa.

“Kwa kushirikiana na Kampuni ya NPK Technology ya jijini Dar es Salaam, Tarura itafunga vifaa za kisasa zikiwemo kamera za CCTV katika mitaa yote ya jiji la Mwanza zitakazonasa na kuratibu shughuli za maegesho na malipo,” amesema Mhandisi Fuko.

Pamoja na malipo ya maegesho, kamera hizo pia zitasaidia masuala ya ulinzi na usalama mitaani kwa kutoa taarifa kwa vyombo husika pindi mienendo inayotiliwa mashaka yanapobainika mitaani.

“Mapato ya ushuru wa maegesho unatarajiwa kupanda kutoka Sh500 milioni za sasa hadi kufikia Sh2.5 bilioni kwa mwaka,” amesema Fuko.

Mfumo huo unaofanyiwa majaribio jijini Mwanza kabla ya kuenezwa nchi nzima pia utasaidia kuimarisha usafi mitaani kwa kubaini maeneo ambayo uchafuz umerundikana na kutoa taarifa kwa mamlaka husika.

Licha ya kuonyesha masikito kwa sehemu ya mapato ya halmashauri kutwaliwa, Mkurugenzi wa Manispaa ya Ilemela, John Wanga amesifia mfumo huo kuhusu upande wa suala la usafi mitaani akisema utasaidia kuyabaini na kutoa taarifa ya maeneo yenye mirundikano ya takataka.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.