• Wasiliana Nasi |
    • Maswali ya Mara kwa Mara |
    • Barua pepe |
    • Malalamiko |
Mwanza Region

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mkoa wa Mwanza

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia ya Mkoa
    • Dira na Dhima
    • Maadili ya Msingi
    • Mikakati
  • Utawala
    • Muundo wa Sekretarieti Mkoa
    • Seksheni
      • Utawala na Rasilimali Watu
      • Mipango na Uratibu
      • Uchumi na Uzalishaji
      • Miundombinu
      • Serikali za Mitaa
      • Afya
      • Elimu
      • Maji
    • Vitengo
      • Fedha na Uhasibu
      • Ukaguzi wa Ndani
      • ununuzi na Ugavi
      • Kitengo cha TEHAMA
      • Kitengo cha Sheria
  • Wilaya
    • Ilemela
    • Nyamagana
    • Magu
    • Misungwi
    • Kwimba
    • Sengerema
    • Ukerewe
  • Halmashauri
    • Halmashauri ya Jiji la Mwanza
    • Halmashauri ya Manispaa ya Ilemela
    • Hamashauri ya Wilaya ya Magu
    • Hamashauri ya Wilaya ya Sengerema
    • Hamashauri ya Wilaya ya Misungwi
    • Hamashauri ya Wilaya ya Kwimba
    • Hamashauri ya Wilaya ya Ukerewe
    • Hamashauri ya Wilaya ya Buchosa
  • Fursa za uwekezaji
    • Miundombinu ya Umwagiliaji na kilimo cha mkataba
    • Kilimo
    • Madini
    • Sekta ya Huduma
  • Huduma zetu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Watumishi
  • Machapisho
    • Mpango Mkakati
    • Ripoti
    • Fomu
    • Miongozo
  • Kituo cha Habari
    • Taarifa Kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya video

TIMIZENI NDOTO ZA RAIS SAMIA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI : KATIBU MKUU TAMISEMI

Posted on: April 5th, 2024

TIMIZENI NDOTO ZA RAIS SAMIA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI : KATIBU MKUU TAMISEMI


Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza Balandya Elikana leo Aprili 5,2024  amefungua rasmi Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Serikali za Mitaa Kanda ya ziwa (LVRLAC) na kutoa rai kwa wajumbe kuhakikisha wanatimiza ndoto za Rais Samia za kuwaletea maendeleo wananchi kutokana na miradi iliyoelekezwa kwenye Halmashauri zao.

Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu (OR-TAMISEMI) Balandya amesema Serikali ya awamu ya sita imeleta miradi mingi hasa mkoa wa Mwanza hivyo ni wajibu kwa wakurugenzi, Meya na Madiwani kuhakikisha miradi hiyo inasimamiwa kikamilifu ili iwe na tija kwa wananchi.

"Ndugu wajumbe wa LAVRLAC Tanzania tuna bahati ya  ziwa Victoria sehemu kubwa kuwa huku kwetu,fursa za uchumi wa bluu umezidi kuongezewa nguvu kwa Serikali kuiboresha sekta ya uvuvi kwa ufugaji wa samaki kutumia vizimba,juhudi hizi ni lazima zilete matokeo chanya kwa usimamizi mzuri kwetu sisi tuliopewa dhamana ya uongozi",amesisitiza mtendaji huyo wa mkoa.

Balandya ameipongeza Jumuiya hiyo kwa juhudi zake za kuziwezesha Halmashauri miradi iliyofikia thamani ya zaidi ya shs bilioni 20 huku ikiendelea na mikakati ya utunzaji mazingira na mapambano dhidi ya mabadiliko ya tabia nchi.

"Hizi safari zenu za mara kwa mara nje ya Tanzania niwasihi mzitumie vizuri kujifunza kutoka kwa webzetu waliopiga hatimua katika utaalamu hasa mabadiliko ya tabia nchi,wananchi wetu wanajikuta wanaharibikiwa na mazao au kutokea kwa ukame,"amesisitiza Balandya.

Mtendaji Mkuu wa LAVRLAC Bill Brown amesema mkutano huo mkuu wajumbe watapata nafasi ya kujadiliana changamoto zilizopo na kuweka mikakati ya kumletea maendeleo mwananchi.

"Wizara hii ya Tamisemi inatengewa fedha nyingi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya maendeleo,hivyo nyie Wakurugenzi na Madiwani tunawahimiza mkasimamie kwa umakini na uadilifu mipango hii ya kuwaletea maendeleo wananchi,"Steven Matambi,Kaimu mkurugenzi wa Serikali za mitaa,Tamisemi.

Washiriki wa mkutano huo  ni wakurugenzi wa Halmashauri,Madiwani,Wenyeviti wa Halmashauri wanatokea mikoa ya Mwanza,Kagera,Simiyu,Mara,Geita na Shinyanga.

Matangazo

  • Tangazo la kukutana na Mhe. Mkuu wa Mkoa wa Mwanza kwa shida mbalimbali. January 08, 2025
  • TANGAZO LA NANENANE TAREHE 8.8.2025 January 08, 2025
  • Angalia zote

Habari Mpya

  • UZALISHAJI ZAO LA PAMBA WAONGEZEKA- MSIGWA

    May 03, 2025
  • DARAJA LA KIGONGO-BUSISI KUANZA KUTUMIKA MUDA WOWOTE KUANZIA SASA.

    May 02, 2025
  • SERIKALI YAANIKA TAKWIMU ZA MAENDELEO YA UTUMISHI YALIYOPATIKANA MWANZA

    May 01, 2025
  • MAKUNDI MAWILI YA MWISHO YALIYOFANYA ZIARA HIFADHI NA JNHPP YAWASILISHA NENO LA SHUKRANI KWA RAS BALANDYA

    April 29, 2025
  • Angalia zote

Video zinazotembea

Siku 365 za Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan Mwanza
video zaidi

Viunganishi vya Haraka

  • Fomu ya Ugonjwa
  • FFARS User Guidelines
  • Miongozo ya mfumo wa bajeti na Mipango
  • Makusanyo ya Ndani ya Halmashauri za Mkoa wa Mwanza
  • PReM
  • Maswali Yaulizwayo Mara kwa Mara
  • Opras fomu
  • OFISI MTANDAO

Viunganishi Linganishi

  • Tovuti ya Ikulu
  • Utumishi
  • Tamisemi
  • Ofisi ya Taifa ya Takwimu Tanzania
  • Idara ya Habari Maelezo
  • Tovuti Kuu ya Serikali

Watembeleaji

world map hits counter

Idadi ya Wasomaji

writingMasterThesis

Ramani ya Eneo

Wasiliana Nasi

    Ofisi ya Mkuu wa Mkoa, Mkoa wa Mwanza, 2 Regional Drive

    S.L.P: 119, Mwanza.

    Simu: 028-2501037

    Simu ya Mkononi: 028-2501037

    Barua Pepe: ras@mwanza.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya faragha
    • Kanusho
    • Ramani ya Tovuti

Hakimiliki©2018. Mkoa wa Mwanza . Haki zote zimehifadhiwa.